Ujenzi wa mabanda ukiendelea katika eneo jipya lililoandaliwa kwa ajili ya mabanda ya kambi ya uvuvi Kemondo. Eneo jipya limeanzishwa ili kupisha utekelezaji wa mradi wa maji na kuepuka uchafuzi wa maji kuzunguka eneo la chanzo.
Baadhi ya wajasiriamali wa samaki katika kambi ya uvuvi ya Kemondo wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Nadhifa Kemikimba (Hayupo pichani), katika kikao kifupi alichopokea maoni yao kuhusu mradi wa maji wa Kemondo.
Mfanyabiashara ya Samaki, katika kambi ya mabanda ya uvuvi-Kemondo, Bi. Christina Wangwi, akitoa maoni yake kuhusu mradi wa maji wa Kemondo ambapo ametoa maoni ya kuongezewa muda zaidi kuwezesha kuhamisha vifaa katika eneo la ujenzi wa chanzo cha maji na kuhamia katika eneo mmbadala ambalo limeshaandaliwa kwa shughuli hiyo ya kuuza samaki.


Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Nadhifa Kemikimba akiwa katika kikao kuhusu mwitikio wa wananchi kuhusu mradi wa maji wa Kemondo na Burhan Mohammed, Mtendaji wa Kijiji cha Rwagati (katikati) na Cyriacus Sosthenes, Mtendaji wa Kata ya Kemondo (kulia). Kushoto ni Mhandisi Lyidia Joseph, Mkurugenzi Msaidizi, Ufuatiliaji na Huduma ya Maji wa Wizara ya Maji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...