


Ulega amesema hayo wakati wa mkutano wa kampeni za Uchaguzi Mkuu katika Kijiji cha Kolagwa kilichopo Kata ya Mipeko ambapo amesema katika wilaya hiyo kuna wawekezaji waliowekeza katika viwanda, hivyo Serikali ya CCM itahaiikisha inasimamia haki na maslahi yaliyowekwa baina ya wafanyakazi, vijiji, halmashauri na taifa ili kupata tija.
Amesema Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020/2025 imeeleza wazi kuhusu haki na maslahi hayo hivyo iwapo wagombea wa CCM watapata kura za ushindi wa kishindo watasimamia hilo.
Amefafanua kwamba Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dk.John Magufuli ndio anajua wawekezaji hao amewatoa wapi hata wakaja kuwekeza katika mkoa huo wa Pwani, hivyo wachague CCM iliwasimamie haki na maslahi hayo.
Aidha kwa upande wa haki zinazotolewa baada ya mfanyakazi kupata ajali Sh.300,000 au ulemavu kazini kulipwa 800,000, amesema CCM inatambua kiasi hicho ni kidogo watashughulikia kuongeza fidia hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...