Mgombea Ubunge Jimbo la Tanga Mjini Ummy Mwalimu amesema endapo atachaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo hilo ndani ya siku 100 atajenga matundu 12 ya vyoo katika Shule ya Msingi Mapambano iliyopo kata ya Magaoni.


Mgombea Ubunge Ummy amesema”Endapo mtanichagua wana Magaoni nitahakikisha Mshahara wangu wa kwanza wa Mwezi Novemba nautumia kwa ajili ya Ujenzi wa matundu ya Vyoo 12 kwa ajili ya Shule ya Msingi Mapambano, ili watoto wetu hususani wakike waweze kupata sehemu nzuri ya kujistiri pindi wanaposhikwa na haja”Amesema Ummy Mwalimu.


Sambamba na hilo Ummy amewaambia pia wana Magaoni kuwa katika kipindi chake Cha Ubunge, atahakikisha anaboresha Miundombinu ya Elimu katika kata ya Magaoni kwa kujenga kupitia mshahara wake  Madarasa mawili   katika shule ya Msingi Magaoni ili kuboresha hali ya Elimu katika shule hiyo, na shule nyingine za Jiji la Tanga kwa kuwa Elimu bora ndio Msingi wa Mafanikio kwa watoto wetu.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...