Na Emmanuel J. Shilatu
Harakati
za kampeni za uchaguzi Mkuu zinashika kasi kuelekea upigaji kura Oktoba
28, 2020. Wagombea wapo wengi ila leo nitawaeleza kwanini Mgombea Urais
kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli achaguliwe tena kuwa Rais wa
Tanzania.
Kwanini tumpe miaka 5 tena Rais Magufuli?
Sababu 5 za kwanini tumchague Dk. Magufuli awe tena Rais wa Tanzania.
Kwanza;
Dkt. Magufuli ndio mgombea pekee kati ya wote mwenye uzoefu wa
kiuongozi kitaifa kwa nafasi ya Rais kwani miaka mitano iliyopita
alikuwa mgeni lakini sasa anauzoefu wa kutosha, anaijua nchi vilivyo
kuliko mgombea yeyote yule. Dkt. John Pombe Magufuli atafanya vizuri
zaidi endapo atapewa miaka mingine ya kuwa Rais wa Tanzania kuliko
mgombea yeyote yule.
Pili;
Haiba yake imebeba uzito na uhalali wa kura yako kwake. Dkt. Magufuli
ni kiongozi mwenye sifa zote za uadilifu, uzalendo, uchapa kazi,
ufuatiliaji na ucha Mungu. Nyota ya Dkt. Magufuli inang'ara zaidi
kutokana na haiba ya matendo na ufanisi wake kiutendaji. Ni uchaguzi
Mkuu wa kumpigia kura kiongozi mchapa kazi, mfuatiliaji, muadilifu asiye
na makando kando, kura ya turufu hapa inamstahili Rais Magufuli.
Tatu;
Kuna kazi kubwa ameianza ya ujenzi wa Taifa anahitaji apewe awamu
nyingine ya miaka mitano aweze kuikamilisha. Rais Magufuli ameanzisha
ujenzi wa miradi ya kimkakati ya kimaendeleo zaidi ya 50 anayohitaji
aongeze muda zaidi aikamilishe tuone matokeo chanya yake. Kumchagua mtu
mwingine ni kuharibu mageuzi haya ya kiuchumi.
Nne;
Rais Magufuli ameyafanya yasiwezekana yawezekane Tanzania. Mathalani
utolewaji wa elimu bure; mapambano ya kweli ya rushwa na ufisadi;
maboresho ya utendaji kazi Serikalini; Utoaji wa huduma kwa jamii mijini
na vijijini mathalani leo hii umeme upo karibia vijiji vyote, maji
mijini na vijijini, huduma bora za afya mpaka maeneo ya vijijini.
Kumchagua mwingine nje ya Rais Magufuli ni kujirudisha nyuma miaka 50.
Tano;
Rais Magufuli ameendeleza vyema misingi iliyowekwa na waasisi wa Taifa
la Tanzania Mwalimu Nyerere na Mzee Karume kwa kuhakikisha anaondoa
matabaka, ukabila, udini na hivyo kuleta umoja, usawa na haki nchini.
Ndio maana leo hii hakuna tena ile kauli ya "unanijua Mimi
nitakupoteza", hakuna tena ubabe na unyanyasaji huo kwa wanyonge.
Kwa
misingi ya kuchagua kiongozi mwenye sifa zote za kuleta maendeleo, Rais
Magufuli ndio suluhisho na matumizi sahihi ya kura yako ya ndio kwake.
Mpe 5 tena Rais Magufuli.
*Shilatu, E.J*
0767488622
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...