Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Sumbawanga (SUWASA) Mhandisi Gibon Nzowa akiwa katika kikao cha dharura na wanafunzi pamoja na jumuiya ya shule ya Msingi ya Kalumbaleza, Halmashauri ya Sumbawanga, kujadili utunzaji wa miundombinu ya maji na matumizi sahihi ya vituo vya kuchota maji. Kikao hicho kimefanyika baada ya uharibifu kufanyika katika kituo cha kuchota maji na kusababisha adha kwa wanafunzi wa shule hiyo.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kalumbaleza, Halmashauri ya Sumbawanga wakiwa na furaha baada ya kupewa ahadi na Mkurugenzi Mtendaji wa SUWASA Mhandisi Gibon Nzowa kuwa huduma ya maji itarejeshwa shuleni hapo ndani ya saa sita, baada ya waharibifu kubomoa mfumo wa majisafi katika kituo cha kuchota maji katika shule yao.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Sumbawanga (SUWASA) Mhandisi Gibon Nzowa akiangalia moja ya kituo cha kuchota maji kilichofanyiwa uharibifu katika shule ya msingi Kalumbaleza. Pamoja na kuhudumia wananchi, kituo hicho kinatoa huduma ya majisafi na salama kwa jumuiya ya shule hiyo na wanafunzi zaidi ya 500.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...