Katibu mkuu-Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii , Jinsia, wazee na watoto, John Jingu akizungumza na vyombo vya habari pamoja na wadau mbalimbali waliohudhuria  hafla hiyo ya maadhimisho ya siku ya mtoto wa kike kuhusu kupinga ukatili dhidi yao na kuweka usawa, yaliofanyika kitaifa Jijini Dar es Salaam.

Katibu mkuu-Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii , Jinsia, wazee na watoto, John Jingu akitembelea mabanda mbalimbali katika hafla hiyo ya maadhimisho ya siku ya mtoto wa kike  yaliofanyika kitaifa Jijini Dar es Salaam.

Na Agness Francis, Michuzi tv

SHIRIKA la utu wa mtoto CDF limeandaa ghafla ya  ya maadhimisho siku ya mtoto wa kike ambapo mgeni rasmi alikuwa ni katibu mkuu-wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto, John Jingu ambapo amesisitiza umuhimu wa  kumlinda mtoto wa kike.

Hayo ameyasema  Katibu mkuu-Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii , Jinsia, wazee na watoto, John Jingu wakati wa  hafla hiyo ya maaadhimisho ya  siku ya mtoto wa kike wakati akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wadau mbalimbali wanaopinga ukatili dhidi ya mtoto wa kike ambapo kitaifa yamefanyika Jijini Dar es Salaam,  Amesema kuwa ipo haja ya kutokomeza  ukatili wa kijinsia hasa  mashuleni.

"Kwa kukabiliana na hili  serikali imeanzisha madawati 155 ya kupinga ukatili wa watoto mashuleni, Ambapo watoto watapata fursa ya kuelezea kwa uhuru kabisa, na walimu wamepewa pia mbinu za kushughulikia changamoto ambazo zinawakabili watoto hao wa kike." Amesema Jingu.

Aidha Mkurugenzi wa shirika la jukwaa la utu wa mtoto CDF, Koshuma Mtengeti ameeleza kuwa ipo haja ya kuwasaidia watoto hao wanaokumbwa na  changamoto ya mimba za utotoni ikiwa asilimia ishirini na saba  kati ya mia hupata ujauzito mashuleni wakiwa na umri chini ya mika 18.

Vile vile Mwanafunzi wa shule ya sekondari Kitunda, Pili Athumani amesema kuwa sheria iliyowekwa na serikali ya kumlinda mtoto wa kike dhidi ya ukatili wa kijinsia itamsaidia mtoto huyo katika kutimiza malengo yake ya hapo baadae.

"Mtoto wa kike atakapoelimishwa sasa na kulindwa dhidi ya madhila hayo ndiye atakayeweza kujenga taifa la kesho." Amesema Pili Athuman.

Hata hivyo Mkurugenzi  mtendaji haki elimu John Kalage amemalizia kwa  kusema kuwa  ili kuondokana na vikwazo hivyo vinavyomsababishia mtoto wa kike kutopata elimu , Ni kujenga usawa wa kijinsia  katika uelimishaji wa watoto.

"Sio watoto wote wa kike wanapata nafasi ya kumaliza elimu ya juu pindi wanapoanza kidato cha 1 wengi wao huishia njiani."Amesema Mkurugenzi mtendaji hakielimu Kalage.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...