Mkurugenzi Michezo, Bw. Yusufu Omar na Mkurugenzi Mkuu wa
Makumbusho ya Taifa, Dkt Noel Lwoga wakitembe ndani ya Uwanja wa
Benjamin Mkapa.
Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa, Dkt. Noel Lwoga
akiwa amesimama na Mkurugenzi wa Michezo, Bw. Yusufu Singo Omar mbele
ya mnara wa kumbukumbu ya ndege iliyoanguka pembeni ya uwanja wa
Uhuru. Mnara huu upo kaskazini mashariki mwa Uwanja wa Taifa, ni mnara
wa kumbukumbu ya marubani wawili wa ndege vita ya Jeshi la Wananchi
Tanzania (JWTZ) ambao ndege yao ilianguka wakati wa maonyesho ya ndege
hizo tarehe 01/09/1980
Mkurugenzi wa Mkuu wa Makumbusho ya Taifa, Dkt. Noel
Lwoga akisalimiana na Mkurugenzi wa Michezo, Bw. Yusufu Omar


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

MAKUMBUSHO ya Taifa la Tanzania kwa kushirikiana na uongozi wa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wameanza mikakati ya kufanya Uwanja wa Taifa kuwa kivutio cha utalii kupitia maonesho ya kihistoria ya uwanja huo.

Hayo yamedhihirika jana baada ya mkutano kati ya Mkurugenzi wa Michezo wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,  Yusuf Singo Omar na Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa, Dr Noel Lwoga ambapo katika mkutano  uliofanyika katika Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es Salaam, ambapo wamejadili masuala mbalimbali ikiwemo la kuanzisha makumbusho ya michezo katika uwanja huo.

Viongozi hao pia wamejadili kuhusu ushirikiano kwenye uhifadhi na kuendeleza malikale na urithi wa utamaduni Tanzania ikiwemo Uwanja wa Uhuru uliojengwa kabla ya Uhuru wa Tanzania (mwaka 1947).

Vile vile walijadili na kukubaliana juu ya kuandaa maonesho au kuanzisha Makumbusho ya Historia ya Michezo Tanzania ambayo yanaweza kuwekwa uwanjani hapo.

Mjadala wao pia ulijikita katika kutumia Uwanja wa Taifa katika kuitangaza Makumbusho ya Taifa na malikale lukuki zilizopo nchini.

Akizungumza baada ya mkutano huo, Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa, Dkt. Noel Lwoga amesema ofisi yake iko tayari kushirikiana na Kurugenzi ya Michezo katika kuvifanya viwanja vya Taifa kuwa vutivu kwa watalii wa ndani na nje ya nchi na kuwa sehemu nzuri ya utalii.

“Tumezungumza vizuri na wenzetu na sisi kama watalaamu wa uhifadhi wa urithi wa asili na utamaduni tutahakikisha viwanja hivi vinavutia watalii kutembelea kabla na baada ya mechi zao,” amesema Dkt. Lwoga.

Amesema jiji la Dar es Salaam lina vivutio vingi vya asili ikiwemo makumbusho, majengo, fukwe, bustani na uwanja wa Taifa na kwamba inahitajika elimu kwa watu kujua viko wapi ili waweze kutembelea.

kwa upande wake, Mkurugenzi wa Michezo,  Yusufu Omar amesema ushirikiano na Makumbusho ya Taifa ni wa muhimu katika kuendeleza malikale nchini ikiwemo Uwanja wa Taifa.

“Sisi kwa upande wetu tumefurahi sana maana ushirikiano huu umekuja wakati muafaka,” alisema Omari.

Amesema uanzishaji wa makumbusho katika Uwanja wa Taifa utasaidia kuleta watu wengi zaidi watakaopenda kuja kujifunza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...