NA FARIDA SAIDY,MOROGORO

Serikali Mkoani Morogoro imewataka wananchi mkoani humo kujiepusha na makundi yoyote yenye viashiria vya uvunjifu wa amani na kufanya vurugu kwenye vituo vya kupigia kura siku ya oktoba 28 mwaka huu. 

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, ambapo amesema Mkoa wa Morogoro umejipanga kuhakikisha ulinzi na usalama katika vituo vya kupigia kura.

Hata hivyo Ole Sanare amewataka wananchi wote waliojiandikisha kupigia kura kwenda kupiga kura siku ya tarehe 28 oktoba 2020 ili kutimiza  takwa la kikatiba la kuchagua madiwani, wabunge na Rais, ambapo zoezi hilo hutokea mara moja ndani ya miaka mitano.

Mkoa wa Morogoro una una jumla ya Majimbo 11,kata 214,huku vituo vya kupigia kura vikiwa 4,774  na waliojiandikisha katika daftari la kudumu la kupiga kura ni 1,623,629.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...