WAWINDAJI, wafugaji na wakulima wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, wamepatiwa elimu ya kufahamu haki zao na kupiga kura ili kuwachagua viongozi wanaowataka.
Mafunzo hayo yametolewa na waelimishaji jamii kupitia  shirika lisilo la kiserikali la Civil Social Protection Foundation (CSP) kwa ufadhili wa shirika la haki za binadamu la Legal Services Facility (LSF).
Muelimishaji jamii wa CSP, Obeid Sarakikya akizungungumza wilayani Simanjiro alisema ili kukuza ushiriki wa kundi hilo kwenye uchaguzi wanapaswa kufahamu haki zao.
Sarakikya alisema wanapaswa kufahamu vituo vya kupigia kura vilivyopo karibu na makazi yao na kutohama kwenye eneo walipo hadi upigaji kura utakapomalizika.
Amesema wanapaswa kujua kikamilifu siku na muda wa kupiga kura ili tuunde wapange ratiba ya shughuli zao mapema kwani huwa wanalisha mifugo mbali na makazi yao.
“Mpiga kura anapiga kura kwenye kituo cha sheria alichosajiliwa na asiyeweza kupiga kura au kutojua kusoma au kuandika anaruhusiwa kwenda na msaidizi  na haruhusiwi kumchagua mtendaji wa uchaguzi,” amesema.
Mwanasheria wa CSP, Eliakim Paul amesema utaratibu wa kupiga kura kwa kutegemea hali ya mazingira ya kila eneo na kupiga kura kituo alichosajiliwa. 
Eliakim amesema mpiga kura anatakiwa kupiga kura kwa amani, utulivu, uhuru na bila kulazimishwa na kupata usaidizi pale wamapohitaji.
Amesema matarajio ya wananchi ni kuona sheria na taratibu zote zinafuatwa kabla, wakati na baada ya kupiga kura, ulinzi na amani unadumishwa na vyombo vya ulinzi na usalama.
“Pia matarajio ya wananchi ni kuona wapiga kura wote wanahudumiwa kwa usawa bila upendeleo isipokuwa kwa wenye uhitaji maalumu,” amesema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...