Mwenyekiti wa (MAREMA)ndugu Jastin Nyari akizungumza na waaandishi was habari leo Ofisini kwake Jijini Arusha Makamu Mwenyekiti wa Madini ya Tanzanite Tanzania Nene John Lyimo
Wa Kwanza kushoto ni Makamu wenyekiti wa Madini ya Tanzanite Tanzania Nene John Lyimo,akiwa na Naibu katibu wa MAREMA mkoa wa Manyara Joseph Bahati



Na.Vero Ignatus,Arusha.

Kamati ya madini ya Tanzanite Tanzania iliyopo chini ya Shirikisho la wachimbaji madini Tanzania( FEMATA )kwa kushirikiana na Chama Cha wachimbaji wa madini mkoa wa Manyara (MAREMA) imetoa pongezi kwa Rais Dkt.John Pombe Magufuli kwa kuchaguliwa kwa awamu nyingine kwa kishindo.

Akizungumza na waaandishi was habari ofisini kwake Mwenyekiti wa (MAREMA)
Jastin Nyari amesema kuwa kazi alizozifanya Dkt.Magufuli katika awamu iliyopita ndiyo imepelekea yeye kuchaguliwa tena .

Nyari amesema kuwa miongoni mwa kazi hizo ni pamoja na ujenzi wa ukuta Mererani,ambapo umesababisha dunia kutambua kuwa Tanzania ndiyo nchi pekee yanapopatikqna madini Tanzanite,tofauti na ulaghai was nchi zilizokuwa zinajipatia ujiko

Sambamba na hayo ufutaji wa Kodi kwa wachimbaji wadogo uliopelekea kupatikana kwa wingi wa madini,Ujenzi wa masoko ya madini ,ambapo mchimbaji akipata madini makubwa Serikali inayanunu tofauti na awali walikuwa hawajui watayauzia wapi

Nyari amesema kuwa kumekuwa na changamoto za vifaa vya kuchimbia madini ,ikiwepo milipuko,ambapo imekuwa ikifika nchini na kupelekwa kwa wachimbaji wadogo wadogo kwa bei ya juu, amemuomba Rais kupitia wasaidizi wake Wizara ya madini na TRA, waangalie uwezekano wa kupunguza gharama ya Kodi, ili wachimbaji waweze kununua vifaa hivyo kwa bei rahisi.

Kwa niamba ya wachimbaji madini Nyari ameiomba Wizara husika iangalie uwezekano wa kutoa kibali , ili Kama wanakosa upande katika kampuni ,kibali kile kimuwezeshe mchimbaji kwenda kununua kwenye kampuni nyingine

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Madini ya Tanzanite Tanzania Nene John Lyimo ,amesema kuwa wanayo matumaini makubwa kwa kuchaguliwa tena kwa Dkt.Magufuli ,wameahidi kufanya kazi kwa bidii ili kuongeza wigo wa walipa Kodi ,kwaajili ya kuongeza pato la Taifa

Aidha ametoa wito kwa Watanzania kutambua kwamba uchaguzi umemalizika ,kilichobakia ni kuongeza bidii katika utendaji, wasibweteke ,waelekeze nguvu zao zaidi katika utendaji kazi kwa manufaa yao,kwa jamii na Taifa kwa kuujenga Uchumi wa Kati, na wa juu zaidi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...