……………………………………………………………………
NA DENIS MLOWE IRINGA, 
MBUNGE wa Jimbo la Makete ,Festo Sanga, ameahidi kuwasomesha watoto 10 kila mwaka elimu ya ufundi ikiwa lengo la kuwapata watalaam mbalimbali watakaosaidia wilaya ya Makete.
Akizungumza wakati wa Mahafali ya Sita (6) ya Chuo cha Ufundi VETA-Makete, Festo Sanga akiwa mgeni rasmi alisema kuwa inasikitisha kuona kati ya wanafunzi 64 wanaohitimu chuoni hapo wengi wao ni wanafunzi kutoka nje ya Makete
 
Hivyo kutokana na hilo alisema kuwa wanafunzi wanaotokea hapa Makete hawafiki 10, zaidi ya 50 wanatoka nje ya Makete (Mara, Tukuyu, Tanga, Dar es Salaaam, Iringa n.). Tafsiri yake ni kushindwa kuitumia fursa hii sisi wanamakete hivyo nitawasomesha wanafunzi kila mwaka.
 
Sanga ambaye ni mdau mkubwa wa michezo nchini alitoa wito kwa  wazazi na walezi kuwapeleka vijana wao chuoni hapo waweze kusoma masomo ya ufundi
Amesema kuwa  Serikali imewekeza mabilioni ya fedha katika chuo hiki pekee cha VETA mkoa wa Njombe, mitambo iliyopo hapa huipati mahali pengine kirahisi hivyo vijana wajitokeze kwa wingi katika kupata elimu ambayo itasaidia maendeleo ya Makete na mkoa wa Njombe kwa ujumla.
 
“Kwa kuanza, mimi kama Mbunge nitakuwa nasomesha wanafunzi 10 kila mwaka kutoka maeneo mbalimbali ya kata zetu ndani ya Makete ambao wanauhitaji na wanamazingira Magumu ya kiuchumi”Amesema
Ameongeza  kuwa kwenye mikutano yote nitaizungumzia VETA MAKETE, kwenye vyombo vya Habari nitaizungumzia na bahati nzuri ada zake ni nafuu na watanzania wengi wanazimudu.
 
Hata hivyo amesema  kuwa  hii ni moja ya fursa ya kupata ujuzi wa mambo mbalimbali kama vile utengenezaji wa batiki, Sabuni, ujenzi wa nyumba, ufundi selemala ufundi magari, umeme majumbani  hivyo vijana watumie vyema uwepo wa chuo hichi.
 
“nimeona BATIKI,SABUNI, Ujenzi wa Nyumba, ufundi selemala, Ufundi magari n.k vitu ambavyo ni fursa kwa vijana wa sasa” Alisema
Mhe.Sanga amesema kuwa anatambua kuna uhaba wa kozi mbali mbali ambazo ni muhimu kama ufundi bomba, ufundi umeme wa magari,ufundi umeme wa majumba hivyo kulichukua na kulifanyia kazi.
 
Wakati huo huo Mbunge Festo Sanga amekabidhi gari kwa wananchi wa Jimbo la Makete kwa ajili ya matumizi mbalimbali ambayo ni msiba,dharula n.k,kuzungukia miradi na utekelezaji wa Ilani kijiji kwa kijiji).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...