Na Pamela Mollel, Longido
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Longido Dkt Jumma Mhina amevitaka vyama vya siasa pamoja na wagombea wao walioshiriki katika uchaguzi Mkuu wa Jimbo hilo kumuunga mkono Mbunge wa Jimbo hilo Steven Lemomo ili aweze kutekeleza mipango ya maendeleo aliyonayo kupitia chama chake na Halmashauri hiyo
Aliyasema hayo juzi wakati akitangaza matokeo ya uchaguzi wa Ubunge katika Jimbo la Longido ambapo alimtangaza Dkt Lemomo kuwa mshindi halali wa jimbo hilo kupitia chama Cha Mapinduzi
Dkt Mhina alisema kuwa vyama vya siasa katika Jimbo hilo kuwa kitu kimoja kwa kuwa uchaguzi umekwisha na Mbunge aliyepita ni wawananchi wote atakaye waletea maendeleo
"Ndugu wananchi baada ya uchaguzi kuna maisha baada ya uchaguzi sisi ni ndugu,sisi ni marafiki,sisi ni Jamii moja tudumishe Amani tuliyonayo"alisema Dkt Mhina
Aidha alisisitiza suala la Amani kama ambavyo Rais John Pombe Magufuli anawasisitizia Watanzania wote
Naye Mkuu wa Wilaya ya Longido Frank Mwaisumbe amesema kuwa Serikali haitasita kumchukulia hatua mtu ambaye atahamasisha au atashiriki kuwa miongoni wataakao anzisha vurugu au maandamano
Mwaisumbe alisema kuwa maandamano hayo hayapo kisheria hivyo mtu au kikundi atachukuliwa hatua kali na Serikali haitafumbia macho Jambo hilo
Aidha alisema kuwa wanaofanya hivyo nikutaka madaraka yasiyo halali
"Tunazo tetesi kwa baadhi ya viongozi walioshindwa katika uchaguzi wameamua kuitisha maandamano ya kuleta vurugu na kuvunja Amani tuliyonayo"Alisema Mwaisumbe
Vyama vya Siasa vilivyoshiriki katika uchaguzi Mkuu nafasi ya Ubunge katika jimbo hilo CCM, Steven Lemomo kura 61,885 , CHADEMA,Lukas Laizer 1,037 ,CUF Kombo Mkadam 65 ,NRA Juma Feruziyson 21
Idadi ya wapiga kura walioandikishwa katika jimbo hilo 76,814,waliopiga kura 63,465,idadi halisi waliopiga kura 63,008,kura zilizokataliwa 457.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Longido Dkt Jumma Mhina
Home
HABARI
MKURUGENZI LONGIDO AVIOMBA VYAMA VYA SIASA VILIVYOSHIRIKI UCHAGUZI KUMUUNGA MKONO MBUNGE MTEULE WA JIMBO HILO ILI KUTEKELEZA MIPANGO YA MAENDELEO KWA WANANCHI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...