Na Zainab Nyamka, Michuzi Tv

MSHAMBULIAJI wa Timu ya Taifa ya Tanzania na Fenerbache, Nahodha Mbwana Ally Samatta atakuwa nje ya dimba kwa muda wa siku 10 baada ya kuumia.

Samatta amepata maumivu ya misuli katika mchezo wake wa mwisho wa Ligi ya Uturuki   dhidi ya Konyaspor wakipoteza kwa goli 2-0.

Baada ya maumivu hayo, Samatta ataukosa mchezo wa kufuzu AFCON kati ya timu yake ya Taifa Tanzania dhidi ya Tunisia utakaochezwa Novemba 13 na Novemba 17 mwaka huu.

Kwa upande wake Samatta amesema,  aliumia katika mechi ya mwisho ya Ligi na alipata maumivu ya misuli na nilifanyiwa vipimo na majibu yametoka mabaya kwahiyo atakuwa nje kwa siku zaidi ya 10.

Amesema, ripoti ya daktari inaelezea kuwa anatakiwa apumzike ili misuli irejee  katika hali ya kawaida.

 Samatta ametoa ya moyoni na kusema, ameumizwa sana kuukosa mchezo huo muhimu kwani alitamani awepo uwanjani kama kiongozi wa timu ila haina jinsi na ameenda kuongea na vijana wa timu pamoja na viongozi ili kuwapa morali ya ushindi.

Kwa sasa timu ipo nchini Uturuki ikijindaa na mchezo wao wa kufuzu AFCON dhidi ya Tunisia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...