Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara, Simba SC hatimaye wamepangwa na timu ya Plateau United ya nchini Nigeria katika mchezo ya awali ya Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF Champions League) msimu wa 2020-2021.

Simba SC itaanzia ugenini nchini Nigeria kati ya Novemba 27-29, 2020 wakati itacheza mchezo wa marudiano nchini Tanzania kati ya Desemba 4-6, 2020.

Katika Droo ya Michuano hiyo ilifanyika jioni ya leo katika Makao Makuu ya Shirikisho la Kandanda Barani Afrika (CAF) mjini Cairo nchini Misri, Simba SC imepangwa na timu hiyo ambapo imeelezwa mshindi kati ya Simba SC na Plateau atacheza na Costa do Sol ya Msumbiji au Platinum ya Zimbabwe.

Wakati huo wawakilishi wa Tanzania katika Michuano ya Kombe la Shirikisho, Namungo FC ya mkoani Lindi watacheza na Al-Rabat Sports Club ya Sudan Kusini katika raundi ya awali ya Michuano hiyo.

Raundi hiyo michezo itapigwa kati ya Novemba 27-29, 2020 na mchezo wa marudiano kupigwa Desemba 4-6, 2020.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...