MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema mvua kubwa Inatarajiwa kunyesha kwa siku tatu mfululizo  kuanzia leo Jumapili Novemba 8,  2020.

Katika Utabiri wao, TMA  imesema mvua  zinatarajiwa kunyesha katikati mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro,Tanga, visiwa vya Mafia, Unguja na Pemba.

Zinatarajiwa kuanza leo hadi Novemba 10, 2020 na  kwamba inatarajiwa maeneo hayo yatakuwa yenye tahadhali kubwa hususani  leo na kesho ambapo vipindi vikubwa vya mvua vinatarajiwa kujitokeza

Aidha TMA wamesema, athari mbali mbali zinaweza kujitokeza ikiwa ni pamoja na mafuriko kwenye makazi ya watu, baadhi ya barabara kufungwa na shughuli za kiuchumi kusimama. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...