Wakili Mkuu wa Serikali Ndg. Gabriel Malata (ambaye alikuwa Naibu Wakili Mkuu wa Serikali) akimkabidhi ofisi kinyaraka Dkt Bonipace Luhende katika hafla fupi iliyofanyika mapema leo ndani ya ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali.

Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Dkt. Boniphace Luhende akitoa neno la shukrani mara baada ya kukabidhiwa rasmi ofisi hiyo kinyaraka mapema leo katika hafla iliyofanyika ndani ya ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali.

Wajumbe wa Menejimenti ya Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, wakimsikiliza Wakili Mkuu wa Serikali Ndg. Gabriel Malata wakati akizungumza nao kabla ya kumkabidhi nyaraka mbalimbali Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Dkt. Boniphace Luhende mapema leo. Kabla ya kuwa Wakili Mkuu wa Serikali Ndg. Malata alikuwa Naibu Wakili Mkuu wa Serikali.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...