EJAZ Bhallo mtunzi na Mwanahistoria ameshiriki na kutoa hotuba katika Semina ya "Single Mother's" iliyoandaliwa na "Save The Society." Ambapo alizungumza juu ya, "mambo mawili ya muhimu ili kufikia malengo," Pia, alikuwa mmoja ya wadhamini wa hafla hiyo.
Kongamano hilo liliwashirikisha "Single Mothers" kutoka sehemu na maeneo mbalimbali nchini Tanzania huku madhumuni ya Semina hii ilikuwa ni kuwaelimisha washiriki kwenye mambo mbalimbali ikiwemo Afya ya Akili, usimamizi wa fedha, sanaa ya uzungumzaji na Ujasiriamali.
Semina hii pia iliwajumuisha wasemaji wengine mashuhuri nchini Tanzania wakiwemo Harris Kapiga (mwandishi wa habari,) Bi. Faiza Ally (Mjasiriamali,) Rodrick Nabe (Mwandishi,) Mr. Bright Motivation (Mhamasishaji,)Selina Condrady (MC) na Dk.Martha Kungu (Mwanasaikolojia na Mwanzilishi wa @afya_passion.)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...