Mwimbaji wa Muziki wa Injili Nchini Tanzania na Katibu wa Umoja wa Wanamuziki Tanzania (TAMUFO), Stella Joel akiwa katika muonekano wa picha tofauti baada ya kuachia wimbo wa kuhamasisha maendeleo unaoitwa Tanzania ya Maendeleo.


 Stella Joel akiwa katika pozi.

 Stella Joel akitafakari ukuu wa Mungu baada ya kutoa wimbo huo ambao unabamba hivi sasa hapa nchini.


Na Dotto Mwaibale


BAADA ya kimya cha muda mrefu, Mwimbaji wa Muziki wa Injili Nchini Tanzania, Stella Joel ameachia wimbo wa kuhamasisha maendeleo unaoitwa Tanzania ya Maendeleo.

Mara ya mwisho Stella aliachia wimbo wa Hakuna Mwanamke mbaya alioshirikiana na malkia wa muziki wa Injili, Rose Muhando.

Stella ambaye ni Katibu wa Umoja wa Wanamuziki Tanzania (TAMUFO) alisema, imefika hatua kwa wasanii kuhamasisha nyimbo zinazochochea maendeleo na kuisaidia jamii kutatua changamoto zake.

“Baada ya Tanzania kufikia uchumi wa kati nikaona ni vyema niweke hilo kwenye muziki, nyimbo za aina hii zinachangia sana kupiga hatua za kimaendeleo zaidi,” alisema Stella.

Stella aliwashauri wanamuziki nchini kubadilisha mtizamo wao, kutojikita kwenye  jumbe za mapenzi peke yake badala yake waangalie changamoto nyingi za kijamii kama masuala ya lishe, ukatili wa kijinsia na mengine.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...