Na Zainab Nyamka, Michuzi Tv

CHUO Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS)  kimempongeza Dkt Harrison Mwakyembe kwa kuteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la chuo hicho.


Pongezi hizo zimetolewa wakati wa mahafali ya kumi na nne (14) tangu Chuo cha MUHAS kiwe Chuo Kikuu kamili mwaka 2007.

Akizungumza wakati wa mahafali hiyo, Makamu Mkuu wa Chuo hicho Profesa Andrea Pembe amesema kuchaguliwa kwa Dkt Mwakyembe wanamuhakikishia ushirikiano mzuri na karibu sana kwa maendeleo ya Chuo na taifa kwa ujumla.

Aidha, Prof Pembe wamemshukuru Mwenyekiti wa Baraza la Chuo aliyemaliza muda wake Mariam Mwaffisi kwa juhudi na utendaji wake wa kazi uliotukuka katika kipindi chote ambacho alihudumu kwenye nafasi hiyo ndani ya baraza la chuo na kukisaidia pindi changamoto zinapotokea na kuweza kufikia hapa walipo.

Dkt Mwakyembe mapema wiki iliyopita aliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Chuo cha MUHAS akichukua nafasi ya Mariam Mwaffisi aliyemaliza muda wake.
Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi  Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Dkt Harrison Mwakyembe akizungumza wakati wa mahafali ya 14 ya Chuo hicho yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...