Katika hotuba yake mbele ya wanaseta na wanabunge, rais wa DRC Felix Tshikedi ametangaza tena nia yake ya kuunda serkali mpya, baada ya kuona serikali ya pamoja aliyoiunda na rais mstaafu Joseph Kabila kushindwa kufanya kazi.

Tshekedi aliamua kuvunja ushirikiano na timu ya rais mstaafu, na sasa anasubiri kuteua mtu ambaye ataweza kujadili na vyama mbalimbali vya kisiasa ili aunde serikali hiyo ambayo ana matumaini ya kwamba mafanikio yake yatatumikia kwa faida ya raia wa DRC.

Disemba mwaka 2019 ndani ya bunge hili lilitangaza ya kwamba mwaka 2020 utakuwa mwaka wa kazi , juhudi zote zilipaswa kufanyika ili kutimiza maendeleo ya nchi.

"Mbele ya raia nilihaidi kufanya mabadiriko nikakubali kutumikia na mtagulizi wangu kupitia muungano ili pamoja tuinue nchi sisi wote kama raia wa nchi hii nzuri , lakini ukweli ni kwamba, lichaya juhudi zangu, nilijitolea, nilikubali hadi kufedheheshwa lakini haikuwezesha muungano huu kuendelea,"rais Tshekedi ameeleza.

Aliongeza kusema; "Kulingana na hali hio ambayo ilikuwa inazuia uongozi wangu ilibidi tu nijibu".

Rais wa nchi hiyo amehaidi kuunda shule ya vita kwa ajili ya maafisa wa jeshi la taifa , huku rais akijaribu kuungwa mkono na jeshi la taifa ambalo kwa sasa linasusiwa kushindwa vita dhidi ya waasi huko mashariki mwa Kongo, Rais amehaidi pia kurejesha mwaka ujao mabaki ya Patrice Lumumba Papa wa uhuru wa taifa ambaye mabaki ya mwili yake yako Ubegiji.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...