Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Aboubakar Kunenge amewataka watanzania kujitokeza kwa wingi kutembelwa maonesho ya Circus Africa yanayoendelea katika Viwanja vya Jeshi Masaki.
Kunenge amefungua rasmi maonesho hayo ya Circus mama Africa na kutoa wito kwa wananchi kutembelea vivutio vya utalii.

Akizungumza baada ya kuzindua, Kunenge ameipongeza bodi ya utalii Tanzania (TTB) kwa kuendelea kuwa wabunifu Katika kuendeleza sekta ya utalii ikiwa ni pamoja na kuweka gharama nafuu ili kuwezesha kila mwananchi kumudu.

Tamasha hilo la Circus mama Africa linahusisha utalii wa michezo ya jukwaani na vivutio vya utalii.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mwendeshaji (TTB) Devotha Mdachi amesema kuwa maonesho hayo yatadumu hadi Januari 10 2021, na yatahusisha michezo mbalimbali.

Amesema, watanzania wajitokeze kwa kwani hii ni michezo yao na inachezwa na watanzania wenyewe kwahiyo waende wenyewe kujionea vipaji halisi.







Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Abubakar Kunenge (katikati) akifurahi pamoja  na Mkurugenzi Mwendeshaji Devotha Mdachi wakati wa uzinduzi wa aonesho ya Circus Mama Africa yanayoendelea katika Viwanja vya Jeshi Masaki.
Kikundi cha maonesho wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Abubakar Kunenge.


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Abubakar Kunenge akizungumza na wageni waalikwa waliofika katika uzinduzi wa maonesho ya Circus Mama Africa yaliyofanyika jana.










Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...