Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimetakiwa kuongeza kasi ya utoaji elimu kwa vitendo  ikiwemo kuboresha mitaala yake ya ufundishaji  ili kuwafanya wanafunzi wanaohitimu katika chuo hicho kujiajiri na kuajiri wengine.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi Teknolojia na   Ubunifu kutoka Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Maulilio  Kipanyula  ambaye amemwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Tekinolojia Dkt. Reonald Akwilapo  katika hafla ya kutoa zawadi kwa wanafunzi wahitimu SUA iliyofanyika Siku ya Alhamisi tarehe 17 Desemba 2020 kwenye ukumbi wa Multipurpose Kampasi ya Edward Moringe.

Prof. Kipanyula amesema kuwa muda muafaka umefika kwa chuo cha SUA kuangalia mitaala inayotumika kufundishia ili iweze kulenga zaidi kwenye kujiajiri.

“Ni wakati muafaka sasa kupunguza idadi ya wahitimu ambao wanamaliza na kuwaza kwenda  kutafuta kazi duniani bali mitaala lazima iwawezeshe wahitimu  waweze kujitegemea na kuzalisha ajira kujiajiri wenyewe na waaajiri watu wengine  ” alisema  Prof. Maulilio  Kipanyula.  

Prof. Kipanyula ameongeza kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi ili kuvisaidia vyuo vikuu nchini viweze kuendelea kuzalisha wataalamu ambao wataweza kulisaidia taifa katika sekta mbalimbali ikiwemo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA Prof. Raphael Chibunda amesema  wanafunzi waliofanya vizuri na kupewa zawadi ni 211 ambao wametoka katika Ndaki na vitivo mbalimbali chuoni hapo ikiwemo wanafunzi bora wa mwaka ambao ni 195 pamoja na Idara sita bora ambazo zimefanya vizuri  kwa kuchapisha katika tovuti

Prof. Chibunda amesema Chuo kitaendelea kutoa zawadi kwa wanafunzi wahitimu waliofanya vizuri kila mwaka katika masomo ili kutambua jitihada wanazofanya nwanafunzi hao ikiwa ni motisha ili wengine nao wafanye vizuri zaidi.

Naye mwanafunzi Bw. Iddy Msangi  wa  mwaka wa pili  katika masomo ya sayansi ya kilimo , ambaye alipata tuzo , alisema  hiyo ni  motisha kwake ya  kuendelea kupambana zaidi  katika kuongeza  bidii  kwenye masomo yake.

“Namshukuru mwenyezi Mungu masomo yalikuwa magumu ila ni kwa uwezo wake Mungu nimekuwa miongoni mwa wanafunzi bora wa mwaka niwashauri wanafunzi wenzangu tunapokuwa chuoni tusome kwa bidii zaidi” alisema Idi Msangi

Kwa upande wake mwanafunzi, Upendo Nzaligo, wa mwaka wa pili  katika  masomo ya  Uandaaji na Uwasilishaji wa taarifa  ambaye alipata tuzo ya Sh 100,000 , alisema ameipokea kwa mikono miwili  na itampatia fursa nzuri kujitangaza  na inatamwongezea  kuongeza juhudi  katika masomo yake.

Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi Teknolojia na   Ubunifu kutoka Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Maulilio  Kipanyula akitoa zawadi kwa wahitimu waliofanya vizuri wakati wa  hafla ya kutoa zawadi kwa wanafunzi wahitimu SUA.
Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi Teknolojia na   Ubunifu kutoka Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Maulilio  Kipanyula  ambaye amemwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Tekinolojia Dkt. Reonald Akwilapo akizungumza na ungozi wa chuo pamoja na Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) hafla ya kutoa zawadi kwa wahitimu hao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...