TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, imeadhimisha siku ya maadili kwa kusikiliza kero za wananchi Vijijini.

Mkuu wa TAKUKURU Wilayani Simanjiro, Adam Kilongozi ametoa elimu ya rushwa na kusikiliza kero za wananchi kwenye Kijiji cha Oiborkishu Kata ya Oljoro namba tano.

Kilongozi amesema wananchi wanapaswa kutoa taarifa za vitendo vya rushwa na dhuluma bila kutishwa na mtu yeyote.

Amesema hivi karibuni wananchi wa eneo hilo walitoa malalamiko yao TAKUKURU kwamba wanachangishwa michango bila kupewa risiti.

Mmoja kati ya wananchi wa eneo hilo Robert Mollel ameipongeza TAKUKURU kwa kufuatilia suala hilo kwani wananchi walikuwa wanachangishwa michango bila kupewa risiti.

Amesema baada ya kutoa taarifa TAKUKURU juu ya kitendo hicho hatua za haraka zimechukuliwa hivyo wananchi kuwa na imani na serikali yao.

Mkuu wa TAKUKURU Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, Adam Kilongozi akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Oirboikishu
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...