Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapt. (Mst) Mhe. George Mkuchika akizungumza na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) – Kampasi ya Tabora (hawapo pichani) alipoenda kukagua jengo jipya la TPSC Kampasi ya Tabora.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapt. (Mst) Mhe. George Mkuchika akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzani-Kampasi ya Tabora alipoenda kukagua jengo jipya la TPSC Kampasi ya Tabora.

Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Emmanuel Shindika akiwasilisha kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapt. (Mst) Mhe. George Mkuchika taarifa ya mradi wa jengo jipya la TPSC-Kampasi ya Tabora alipoenda kukagua jingo hilo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapt. (Mst) Mhe. George Mkuchika akishuhudia mpangilio wa vitabu katika maktaba maalum iliyoko kwenye jengo jipya la Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) – Kampasi ya Tabora.

 Baadhi ya wanafunzi wakipata mafunzo katika moja ya darasa lililopo ndani ya jengo jipya la Chuo Cha Utumishi wa Tanzania (TPSC) -Kampasi ya Tabora lililojengwa kwa fedha za mapato ya ndani. Mwonekano wa jengo jipya la Chuo Cha Utumishi wa Tanzania (TPSC) – Kampasi ya Tabora lililojengwa kwa fedha za mapato ya ndani.

***********************************

Na. James K. Mwanamyoto – Tabora

Tarehe 17 Disemba, 2020

Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) kimepongezwa kwa kutumia fedha za mapato yake ya ndani kiasi cha shilingi bilioni 3.5 kujenga jengo la ghorofa mbili lililoanza kutumika kutoa mafunzo kwa Watumishi wa Umma na Wananchi katika fani mbalimbali zinazotolewa na chuo hicho kwenye Kampasi ya Tabora.

Pongezi hizo zimetolewa leo Mkoani Tabora na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapt. (Mst) Mhe. George H. Mkuchika mara baada ya kukagua jengo jipya la TPSC Kampasi ya Tabora.

Mhe. Mkuchika amesema hatua ya kutumia fedha za ndani kujenga jengo lenye ofisi na madarasa, linapaswa kuigwa na taasisi nyingine za umma ambazo zinaitegemea Serikali kuwapatia fedha kuboresha ofisi zao.

“Kitendo cha kutumia fedha za ndani kwa maendeleo ya taifa ni jambo zuri ambalo Mhe. Rais amekuwa akisisitiza mara kwa mara, hivyo, ujenzi wa jengo hili linanipa ujasiri wa kuwaalika Viongozi wa Kitaifa kulizindua rasmi, huku kipaumbele kikiwa kwa Mhe. Rais mwenyewe,” Mhe. Mkuchika amefafanua.

Mhe. Mkuchika ameongeza kuwa, ushirikiano na uadilifu uliopo baina ya Viongozi na Watumishi ndio ulifanikisha kukamilika kwa ujenzi wa jengo hilo, hivyo amewataka kuuendelea na utamaduni huo kwa masilahi ya chuo na maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Akitoa taarifa kuhusu ujenzi wa jengo hilo, Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Emmanuel Shindika amesema jengo hilo limekamilika na kuanza kutumika kabla ya uzinduzi rasmi ili kuongeza ufanisi kiutendaji na kubaini mapungufu yanayoweza kujitokeza kwa lengo la kuyadhibiti.

Mradi wa ujenzi wa jengo hilo linalojumuisha maktaba, vyumba vya madarasa ya kompyuta, kumbi, madarasa ya kawaida na ofisi za watumishi ulianza tarehe 5 Novemba, 2014 na kukamilika rasmi tarehe 26 Machi, 2020.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...