Na Amiri Kilagalila, Njombe
RAINARY Lugome mkazi wa wilaya ya Ludewa mkoani Njombe ameuawa na ndugu yake aliyefahamika kwa jina la Claus Samweli Lugome (46) kwa tuhuma za kuku wake kuingia katika shamba la kaka yake.

Akizungumza na vyombo vya habari kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Hamis Issa amesema wanawashikilia wanafamilia wawili akiwemo baba wa watoto hao, Ado Samweli Lugome pamoja na kijana aliyehusika na mauaji kwa ajili ya upelelezi.

“Haya mauaji ni ya hovyo,yaani kaka kamuua mdogo wake kisa na mkasa kuku wa mdogo mtu wameenda kwenye shamba la kaka mtu.”Alisema Kamanda Issa

Hata hivyo ameongeza kuwa katika upelelezi uliokuwa unaendelea wamebaini familia hizo zimekuwa zikituhumiana na maswala ya ushirikina.

“Katika ufuatiliaji wa swala hili tumeona wanatuhumiana kuwa mmoja anatembea na mke wake na mwingine anamtuhumu mwenzie kuwa alikuwa anamloga.”Alisema kamanda Issa

Ametoa rai kwa jamii kuacha kuamini ushirikina badala yake kutoa taarifa sehemu husika ili kusaidiwa kuliko kuchukua hatua mkononi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...