Diwani wa Kata ya Mabwepande Mhajilina Kassim  (kulia) akiongoza wananchi kufanya usafi katika eneo  itakapojengwa Shule ya Msingi Bunju B.


Diwani wa Kata ya Mabwepande Mhajilina Kassim 'Obama'  (wa pili kushoto) akiongoza wananchi kufanya msako wa nyoka aina ya chatu wanaodaiwa kutishia usalama wa wananchi wa eneo la Kitunda, Mtaaa wa Bunju B.


Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam

WANANCHI  wa eneo la Kitunda  Mtaa wa  Bunju B, Kata   ya Mabwepande, Kinondoni, Jijini Dar es Salaam,  wameiomba serikali kuwasaidia baada ya kuishi  kwa hofu kutokana na tishio la chatu.

 Wananchi hao walitoa kilio hicho leo  katika kikao kilichoitishwa na Diwani wa Kata ya Mabwepande Mhajilina Kassim  maarufu kama Obama.

Mkutano huo ulianza kwa wananchi  hao   kufanya usafi katika eneo  itakapojengwa Shule ya  Msingi Bunju B  ambapo walifyeka eneo hilo ili kuanza ujenzi.

Pia  wakiongozwa na diwani huyo walifanya msako wa chatu kwa kutumia silaha mbalimbali za jadi.

Walisema  licha ya chatu  pia   kwenye eneo   hilo wameonekana wanyama wakali  kama vile chui na mamba.

Akizungumza na wananchi hao, Diwani Kassim  alisema  anamini serikali ni sikivu  itawasaidia  kukabiliana na tishio la  chatu hao wanaodaiwa  kuzagaa  mtaani.

Obama aliszema chanzo cha kuzaliana kwa chatu  na wanyama wakali katika eneo  hilo ni kuwepo kwa pori ambalo lina mgogoro  kwa miaka zaidi ya saba.

Alisema pori  hili  liko karibu na eneo   ambalo shule  ya msingi itajengwa, hivyo kuiomba serikali kuingilia kati ili kesi  ya mgogoro wa eneo hilo iliyopo Mahakama Kuu ya Ardhi  kumalizika.

“Hatuna mamlaka ya kuingilia kati kesi ila tutaiandikia maombi mahakama ituruhusu kufyeka eneo hili ili kuepusha chatu kuzaliana,”alieleza Obama.

Alisema tayari  Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni imetoa  sh. milioni  156 kujenga madarasa tisa  katika eneo hilo.

 “Hatuna shule hapa Kitunda,  shule ipo upande wa pili wa  Barabara  ya Bagamoyo, Mtaa wa Kiyonzile, hivyo ujenzi wa shule hii mpya ni muhimu ili kuepusha watoto kugongwa na magari au tishio hili la chatu na wanyama wakali. 

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Bunju B, Athuman Njama ,  alithibitisha wananchi wake kuishi katika tishio la chatu hao aliodai wanalanda mara kwa mara mtaani.

“Wananchi wanaishi kwa hofu  hapa.Wengi wanajifungia  mapema ndani,”alisema Njama.

Aliongeza: “Tunaomba serikali ije itusaidie kuwinda wanyama hawa.”

Mzee  Asheli Ishiriyo, mkazi wa eneo hilo  alisema hivi karibuni chatu mkubwa  alikutwa akimmeza mbwa katika banda la jirani yake.

“Alikuwa ni mkubwa kama nguzo ya umeme. Alipo tuona alimtema mbwa na kutuvimbia ili kukabiliana na sisi. Tukakimbia,”alieleza mzee huyo.

Ally Said, alisema  mwezi mmoja uliopita walifanikiwa kumuua chatu mmoja na kumfukia.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...