RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhi Cheti cha
Heshima Mshiriki namba moja wa Mazoezi Zanzibar, akikabidhiwa na
Mwenyekiti wa Chama Cha Mazoezi ya Viungo Zanzibar (ZABESA) Ndg.Said
Suleiman, wakati wa hafla ya mazoezi ya viungo ya pamoja yaliofanyika
katikia Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar leo 1-1-2021.(Picha na Ikulu)
WASHIRIKI wa Tamasha la Mazoezi ya Viungo Kitaifa Zanzibar Bi. Pili
Mwalimu (kulia) na Bi.Kazija Othman wakimaliza matembezi ya Tamasha la
Kitaifa la Mazoezi ya Viungo Zanzibar wakipita katikja jukwaa kuu la
Viongozi katika Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar kumalizia matembezi hayo
yalioazia katika viwanja vya Mapinduzi Square Michezani kisonge na
kumalizia Uwanja wa Amaan kwa mazoezi ya pamoja.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akishiriki katika Tamasha
la Mazoezi ya Kitaifa ya Viungo Zanzibar na (kushoto kwa Rais) Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla na Mkewe Mama
Sharifa Omar Khalfan (kulia kwa Rais) Spika wa Baraza la Wawakilishi
Zanzibar Mhe.Zuberi Ali Maulid, Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Maryam
Mwinyi na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Idrisa Kitwana
Mustafa wakishirika katika Tamasha la matembezi ya mazoezi ya Viungo
Zanzibar, yalioazia katika viwanja vya Mapinduzi Square Michezani
Kisonge Jijini Zanzibar na kumalizia katika Uwanja wa Amaan.(Picha na
Ikulu)
WASHIRIki wa Tamasha la Mazoezi
ya Viungo la Kitaifa Zanzibar wakipita katika jukwaa kuu la Viongozi
wakati wa kumalizia matembezi hayo katika viwanja vya Amaani na
kujumuika katika mazoezi ya pamoja yaliofanyika katika uwanja huo leo
1-1-2021.(Picha na Ikulu)
WAFANYAKAZI wa Benki ya NMB Tawi
la Zanzibar wakishiriki katika Tamasha la Mazoezi ya Viungo la Kitaifa
Zanzibar wakipita katika Jukwaa la Viongozi katika Uwanja wa Amaan,
matembezi hayo ya mazoezi ya Viungo Zanzibar yamepokelewa na Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi
(hayupo pichani) na kujumuika katika mazoezi ya pamoja yaliofanyika
katika Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)
WANAMICHEZO wa Kikundi cha mazoezi
ya Viungo kutoka Mkoani Dodoma wakishiriki katika Tamasha la Mazoezi ya
Viungo la Kitaifa Zanzibar wakipita katika jukwaa kuu la Viongozi
wakati wa kumalizia matembezi hayo na kupokelewa na Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi (hayupo
pichani) na kujumuika katika mazoezi ya pamoja yaliofanyika katika
Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi na (kushoto kwa Rais)
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad na
(kulia kwa Rais) Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Zuberi Ali
Maulid, wakishiriki katika mazoezi ya pamoja ya viungo yakiongozwa na
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo Ndg. Omar
Hassan King, baada ya kumaliza matembezi hayo katika viwanja vya Amaan
Jijini Zanzibar, wakati wa Tamasha la Kitaifa la Mazoezi ya Viungo
Zanzibar lililofanyika leo 1-1-2021.(Picha na Ikulu)MSHIRIKI
wa Mazoezi ya Viungo Zanzibar Bi. Halima Muhamad Othman (60) kutoka
Kikundi cha Mazoezi cha Solution Fitness Club cha Magogoni Zanzibar
akishiriki katika mazoezi hayo yaliofanyika katika Uwanja wa Amaan
Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...