Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Alinanuswe Kabungo akizungumza na wadau wa vyombo vya Utangazaji , Vyuo vya Uandishi wa Habari ,Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) pamoja na NACTE katika mkutano wa kujadili mitaala ya Uandishi wa Habari  uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Leseni  za Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mhandisi Andrew Kisaka akitoa maelezo kuhusiana na mkutano wadau vya Utangazaji na Vyuo vya Uandishi wa Habari uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Mhariri wa Azam Media Group Yahya Mohamed akichangia mjadala katika mkutano wa kujadili mitaala inayoakisi Sekta ya utangazaji iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).
Badhi ya wadau wakifatilia mjadala kuhusiana na mtaala wa Uandishi wa Habari.


*Mjadala  Mtaala  kuwaandaa waandishi waibua maswali mengi

Na Chalila Kibuda,Michuzi TV

SERIKALI imetakiwa kuandaa mitaala ya uandishi wa habari  inayoakisi soko ili kusaidia vijana wanaotoka vyuoni kufanya kazi kwa ufanisi na kuendana na hali halisi pamoja na kukabiliana na changamoto za utendaji.

Akizungumza jijini jana  kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini TCRA Alinanuswe Kabungo  katika  ufunguzi mkutano wa pamoja wa vituo vya utangazaji,vyuo vya uandishi wa habari na taasisi zinazohusika na uandaaji wa mitaala alisema  ushauri huo ulitolewa  na  wadau wa habari nchini wanaofanya kazi katika vyombo vya habari kupitia vikao mbalimbali walivyokaa na mamlaka hiyo.

Alisema vijana wanaoajiriwa kutoka vyuoni hata wale waliopo kwenye ajira wamekiri kutofundishwa wala kudokezwa masuala yanayohusu sheria na kanuni zinasimamia sekta ya utangazaji.

"Uandishi wa habari haiakisi hali halisi ya soko na kufanya utendaji  kazi wa vijana hawa kukabiliana na changamoto nyingi za kiutendaji,"amesema Kabungo.

Amesema  teknolojia ya habari na mawasiliano imebadilika kwa kasi hivyo uandaaji wa habari uchakataji wa habari na uwasilishaji wa habari  kwa wananchi unabadilika.

Ameema hakuna semina,warsha,makongamano yanayoratibiwa na vyuo au wasimamizi na vyuo kujadili masuala yanayohusu maendeleo ya sekta ya habari na mabadiliko yanayotokea kwenye soko.

Kabungo amesema  TCRA ina jukumu la kuhakikisha kuwa kunakuwepo na ufanisi mkubwa kwenye sekta ya utangazaji katika   wanajenga nyumba moja.

Naye muhadhili wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino(SAUT) Dotto Bulembu alisema  mitaala ya vyuo inaandaliwa na serikali hivyo ni vizuri serikali inapaswa kushirikisha wadau ili kujua mahitaji ya wanataaluma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...