Mheshimiwa waziri wa maji nishati na madini-ZNZ..Suleiman Makame..Mkurugenzi Mkuu-ZAWA- Mussa Ramadhan Haji,kulia ni Angelica Pesha-Mkuu wa Kitengo cha Fedha Tigo pesa.

 ====   ======  =======

MAMLAKA ya Maji Visiwani Zanzibar (ZAWA), kwa kushirikiana na Kampuni ya Simu za Mkononi, wameingia makubaliano ambapo wateja wataanza kulipa bili za maji kwa kupitia Tigo Pesa.

Akizungumza Visiwani hapa, Kaimu Afisa Mkuu wa Kitengo cha Tigo Pesa, Angelica Pesha, alisema kuwa lengo la kampuni hiyo ni kuhakikisha watu wanabadilisisha maisha na kuishi kidijitali kwa kutumia Tigo Pesa kupata huduma mbalimbali ikiwemo kulipa bili kirahisi.

“Tumejikita katika kuhakikisha wateja wanaishi maisha ya kidijitali kupitia Tigo Pesa katika kupata huduma za mahitaji ya kila siku. Kwa kuingia makubaliano haya na ZAWA, ni hatua nyingine itakayowasaidia wateja wetu kulipa bili zao kirahisi,” alisema Angelica.

Aliongeza: "Hapo awali wateja walikuwa wakilazimika kufika katika ofisi za ZAWA na wale waliochelewa kulipa bili walikuwa wakikatiwa huduma, kwa sasa kupitia simu yako ya mkononi una uhakika wa kulipa bili za maji kwa kutumia Tigo Pesa.”

Mkurugenzi wa ZAWA, Mussa Ramadhan, ameishukuru Tigo kwa kuchukua hatua hiyo Visiwani Zanzibar ambapo wateja wataanza kuliba bili zao kirahisi na kuendele kupata huduma ya maji.

“Mikakati yetu ni kuendeleza na kurahisisha huduma ya maji kwa wateja wetu, hivyo Tigo Pesa itarahisisha ukusanyanyaji wa bili kwa haraka kupitia simu za mkononi," alisema.

Alisema kuwa suluhisho hilo linatarajiwa kuharakisha ufanisi katika ukusanyaji wa mapato kwa mamlaka na hivyo kuongeza uwezo wake kwenye utoaji wa huduma ikiwa ni pamoja na uboreshaji wa miundombinu ya maji na kupanua wigo wake ndani ya Visiwa hivyo.

Alisema maji ni moja ya rasilimali muhimu katika kuendesha shughuli za nyumbani na za kiuchumi.

 Mamlaka ya Maji ya Zanzibar ina jukumu kubwa la kusimamia huduma za usambazaji maji kwa zaidi ya walengwa 1,161,915 katika Visiwa hivyo.

Kulipa bili mteja atatakiwa kupiga *150*01# alafu anachagua namba 4 Kulipa Bili, atabonyeza namba 3 na kuingiza namba za biashara (123569), kisha zitafuatiwa na namba za akaunti ya ZAHA baadaye namba ya siri ya Tigo Pesa kwa uthibitisho na moja kwa moja atapokea ujumbe mfupi wa maneno.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...