MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa kushirikiana na jeshi la Polisi wanamshikilia mwanaharakati Joyce Kiria kwa kosa la kuendesha mtandao wa Youtube bila kuwa na leseni.

Hatua hiyo ni muendelezo wa Mamlaka hiyo katika kudhibiti  Mawasiliano kwa watu wanaondesha maudhui kwa njia ya Mtandao, pamoja na  kutoa elimu kwa watu wanaoendesha maudhui mtandaoni kujisajili katika Mamlaka hiyo.

Mbali na Joyce Kiria TCRA kwa kushirikiana na polisi wamemkamata  mtu mmoja  kwa kuendesha Chaneli ya Youtube bila usajili.

 Joyce Kiria anashikiliwa na Polisi katika kituo cha Polisi Mabatini Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...