Na Woinde Shizza ,  Michuzi Tv -ARUSHA


Mkuu wa mkoa wa Arusha Iddi Kimanta amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muunganano wa Tanzania Dkt  John Pombe Magufuli kwa kutoa ndege ya serikali kubeba mwili wa aliyekuwa Katibu Tawala wa mkoa wa Arusha Richard Kwitega kuelekea kwenye maziko jijini mwanza.

Akitoa ratiba ya kuaaga mwili kwa waandishi wa habari, Kimanta alisema kuwa Rais Magufuli ameonesha kuthamini utendaji wake wa kazi na ameonesha heshima kubwa kwa kiongozi mwenzao.

Alisema ratiba  ya kuaga na kuelekea kwenye maziko itaanza  kesho Ijumaa asubuhi ambapo majira ya 7:50  mwili utachukuliwa katika chumba Cha kuhifadhia maiti na kupelekwa nyumbani kwake na baada hapo wataondoka nyumbani na kwenda katika kanisa la mtakatifu Theresa kwa ajili ya misa.

Alisema  Misa itaanza  saa mbili kamili asubuhi hadi saa tatu na baada ya hapo wataondoka kuelekea uwanja wa Sheikh Amri Abeid   kwa ajili ya hotuba ya Mkuu wa mkoa na Salamu mbalimbali za rambirambi ambazo zitaambatana na kuaga mwili wa marehemu na  zoezi hilo  litaanza saa 9:25 asubuhi hadi saa 1:30 mchana na baada ya hapo maandalizi ya kwenda uwanja wa ndege wa Arusha yataanzaa na wanatarajia kuondoka majira ya saa 3: 00 alasiri kwenda mwanza.

Alifafanua kuwa baada ya kufika jijini Mwanza mwili utapelekwa nyumbani kwake Buswalo ambapo utalala hadi asubuhi, ambapo majirani  watapata wasaa wa kuaga na baada ya hapo wataelekea Wilaya ya Sengerema Katika kijiji cha Ngoma  ambapo ndiko alipozaliwa kwa ajili ya ibada na maziko ambayo yatafanyika Alasiri siku ya Jumamosi.
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. Iddi Kimanta




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...