Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Godwin Gondwe amewataka wamiliki wa Bar na  kumbi za  starehe kufanya biashara kulingana na vibali wanavyopewa na Manispaa.

Ameyasema hayo leo wakati wa ziara yake ya kutembelea miradi mbalimbali ya Kijamii ndani ya Wilaya ya Temeke.

Akizungumza na wananchi wa  Mtaa wa Moringe Kata ya Mbagala, Gondwe amesema wamiliki wote wanatakiwa wafuate vibali vyao kama walivyoelekezwa na Manispaa ili kuondoa kero kwa wananchi wanaoishi maeneo ya karibu.

Gondwe amesema, kila kumbi ya starehe ina kibali chake kuna waliopewa vya kukesha hadi asubuhi, kuna wengine wamepewa mwisho muda fulani ila wapo wanaokikuka na ni kosa kisheria.

Amesema, " Kuna kumbi zinapiga muziki hadi asubuh wakiwa hawana vibali hivyo na wanatoa kero kwa wananchi kuna wengine ni wagonjwa, wanataka kupumzika na hili suala nataka watendaji wa mtaa mlifanyie kazi sitaki kusikia lawama tena za wananchi,"

Gondwe amesema, kama mmiliki amepewa kibali cha kupiga muziki hadi asubuh lakini amekuwa anashindwa kufuata masharti yanayotakiwa na kama Manispaa tukiona mtu anafanya hivyo tutamnyang'anya kibali hicho.

Mbali na hilo, Gondwe amewataka maafisa Mazingira wa Kata kusimamia mazingira ipasavyo na kuwachukulia hatua kali za kisheria wamiliki wa Viwanda vinavyotiririsha maji machafu kwenye makazi ya wananchi.

Hilo, ni kutokana na wananchi wa Kata ya Mbagala kulalamika utiririshwaji wa maji machafu kutoka katika viwanda vilivyopo karibu na maeneo ya wananchi kikiwemo Kiwanda cha Sabuni.

Aidha, ametoa maagizo hayo kwa viwanda hivyo kuacha haraka tabia hiyo.

 
 
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Godwin Gondwe akizungumza na wananchi wa kata ya Mbagala baada ya kupokea malalamiko ya kumbi za starehe kupiga muziki mkubwa na kuwa kero kwa wananchi sambamba na uharibifu wa mazingira kutoka kwenye Viwanda.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...