Akikabidhi kitabu cha maombolezo Mhe.Mgonya amesema kuwa kitabu hicho kitazunguka katika Taasisi zote zilizopo wilaya ya Mvomero kwa kipindi cha siku 21 za maombolezo, na kwamba Chuo Kikuu Mzumbe ndiyo taasisi inayozindua utaratibu huo ambapo kitabu hicho kitakaa chuoni hapo kwa muda wa siku tatu mfululizo.
Mhe.Mgonya amesema Hayati Dkt.John Pombe Magufuli alikuwa ni Kiongozi Mzalendo, Mchapakazi, Mwadilifu na aliyependa sana nchi yake na kwamba watanzania wote tunao wajibu wa kuyaenzi na kuyatekeleza mema yote aliyotuachia.
Akipokea kitabu hicho Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo, Prof.Ganka Nyamsogoro amesema Chuo Kikuu Mzumbe kimepokea kwa masikitiko makubwa msiba wa Hayati Dkt. Magufuli na kueleza katika muda mfupi aliohudumu alifanya uwekezaji mkubwa katika miradi ya maendeleo ikiwemo Sekta ya elimu, na kwamba Chuo kikuu Mzumbe ni miongoni mwa Taasisi zilizonufaika na uwekezaji huo ukiwemo uwekezaji mkubwa katika ujenzi wa mabweni na majengo ya madarasa.
Prof Nyamsogo aliongeza kuwa Chuo kimepokea kwa heshima kubwa kitabu hicho cha maombolezo cha Wilaya na kwamba Wanajumuiya wa Chuo Kikuu Mzumbe watazitumia vyema siku tatu za kusaini kitabu hicho, kwani wanautambua vyema mchango mkubwa uliotolewa na Hayati Dkt.Magufuli.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...