NA FARIDA SAID MOROGORO.


Kuelekea Mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhan, Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Abdal aziz Abood amekutana na watoto yatima, wazee wasiojiweza pamoja na watu wenye ulemavu walio chini ya taasisi ya Ukumbusho wa Zaka Tanzania yenye makao makuu yake Mkoani Morogoro na kuahidi kusaidia futari katika kipindi chote cha mwezi wa Ramadhan.
 
Mhe, ABOOD amekutana na makundi hayo katika Kongamano la kukaribisha mwezi  mtukufu wa Ramadhan lililo andaliwa na Taasisi ya kiraia ya Ukumbusho wa Zaka Tanzania, inayowasaidia watu wenye mahitaji mbalimbli, wakiwemo watoto yatima,Watu wenyeulemavu pamoja na wazee wasio jiweza.
 
Akizungumza katika kongamano hilo Mhe Abood amesema pamoja na kuchangia futari katika kipindi chote cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani lakini pia atatoa mavazi kwa vijana 80 wanalelewa na taasisi hiyo katika siku kuu ya EDD ELFITRI ili wawezi kufurahia sikuku hiyo kama vijana wengine.
 
“Mimi kama Mbunge wenu nawapatia mavazi ya kusherekea siku kuu ya Edd watoto wote yatima ambao nimeambia idadi yao ni 80 waliopo hapa kwenye jumuiya ya Ukumbusho wa Zaka Tanzania  na nitaendelea kushirikiana nanyi kwa kila jambo.”Alisema Mhe Abood.
 
Wakati huo huo Mhe Abood amekabidhi kitimwendo kwa taasisi ya Ukumbusho wa Zaka kitakacho wasaidia watoto wenye ulemavu wanao lelewa na taasisi hiyo, ambao awali walikuwa na uhitaji wa kiti hicho kinacho wasaidia kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine.
 
“Kutoa msaada kwa watu wasio jiweza ni moja ya njia ya kupata thawabu, lakini pia kunasaidia kudumisha upendo kwa ndugu na jamaa zetu, na ndio maana hata kwenye Quaran tukufu na vitabu vingine vya dini vimeandika na mwenyezi mungu ametuamrisha kuwasaidia watoto yatima na watu wasio na uwezo.”Alisema Mhe Abood.
 
Awali akiwasilisha changamoto zinazo wakabili katika jumuiya hiyo kwa Mbunge wa jimbo la Morogoro Mjini Mhe Abdalaziz Abood ,Mwenyekiti wa Jumuiya Sheikh Omari Mahmudu Katura amemuomba Mhe ABOOD awasaidie kuwatafutia wahisani watakao weza kuwasaidia makundi hayo ya watu wenye uhitaji .
 
Pia wamewataka watanzaia kutoa misaada katika vituo maalumu vya kulelea watoto yatima na watu wasiojiweza, kwani kufanya hivyo  kutasidia kufikia kundi kubwa zaidi kuliko kutoa kwa mtu mmoj mmoja.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...