Na Mwamvua Mwinyi,Rufiji


Timu ya Wanafunzi wa vyuo vikuu nchini kutoka katika baadhi ya vyuo  ,wametembelea mradi mkubwa wa bwawa la kufua umeme la mwalimu Nyerere liliko Rufiji mkoani Pwani ,ili kujifunza na kujionea kazi iliyofanywa na serikali awamu ya tano  kipindi cha Hayati Rais Dkt. JOHN POMBE MAGUFULI.

Akizungumza mara baada kutembelea mradi huo , Rais wa serikali ya wanafunzi wa chuo kikuu cha sayansi na teknolojia cha Mbeya HILARY LOOKEN ambao ndio walioandaa ziara hiyo, anasema mbali ya kujifunza kivitendo lakini pia wanasapoti juhudi za serikali awamu ya tano katika kuipeleka Tanzania  katika viwango vikubwa vya kiuchumi kwani mradi huo  pamoja na faida nyingi utaeza kuwanufaisha watanzania katika nyanja mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuhifadhi mazingira.

" Tumeona tuje kujifunza katika mradi huu kwani katika chuo chetu  tuna fani mbalimbali zinazotolewa ikiwa ni pamoja na Fani ya uinjinia,  hivyo wanafunzi wamejifunza mengi katika mradi, na niseme tu naipongeza serikali kwa kufanya mradi huu mkubwa wa kimkakati ambao utakwenda kutupeleka katika viwango vingine kiuchumi," 

Alisema HILLARY LOOKEN , Rais wa Serikali ya Wanafunzi  chuo cha Sayansi  sayansi na teknolojia cha Mbeya (MUST).  
 
Mradi huu unajengwa na mkandarasi wa kampuni ya Arab Contractor kutoka Misri utagharimu kiasi cha Trilioni 6.5 na unatarajiwa kujengwa kwa kipindi cha miezi kati ya 36 mpaka 42 ya ukamilishaji wa mradi huo.

Kukamilika kwa utekelezaji wa mradi wa ujenzi, kutaiwezesha Tanzania kuzalisha kiasi kikubwa cha umeme kitachokasaidia kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo ujenzi wa uchumi wa viwanda na mradi wa reli ya kisasa,.

Mhandisi DAVID MUNKALA  ni  Mtaalamu wa Maji wa Mradi wa Julius Nyerere,  alisema Utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa bwawa la kufua umeme wa maji la Julius Nyerere kwenye bonde la mto Rufiji unaendelea kwa kasi inayohitajika na kuwa unatarajiwa kukamilika kipindi cha mkataba uliosaniwa.
 

BAADHI YA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU KIKIWEMO  CHA SAYANSI NA TEKNOLOJIA MBEYA (MUST) WAKIMSIKILIZA MHANDISI DAVID MUNKYALA (KATIKATI) AMBAYE NI MTAALAMU WA MAJI KATIKA MRADI WA BWAWA LA KUFUA UMEME LA MWALIMU NYERERE LILILOKO RUFIJI, WAKATI WALIPOTEMBELEA MRADI HUO WA KIMKAKATI UNATEKELEZWA NA SERIKALI  KWA ASILIMIA 100, ILI WAWEZE KUJIFUNZA NA KUJIONEA MAENDELEO YA MRADI HUO.(Picha na Mwamvua Mwinyi)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...