………………………………………………………………………………
Katibu Mkuu wa wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi amewataka Waandishi wa Habari nchini  kutekeleza majukumu yao kwa weledi ili kuepuka makosa ya kisheria yanayoweza kujitokeza.
Dkt. Abbasi ameyasema hayo leo jijini Dodoma alipokuwa akitoa mada juu ya ”Matumizi ya Mitandao ya Kijamii”’ wakati wa mafunzo kwa Waandishi wa Habari za mtandaoni wa Shirika la Utangazaji Tanzania  (TBC) (TBConline).
Amewataka kutojiona wanyonge kwa kufanya kazi hiyo,  bali wajione watu waliobeba dhamana kubwa katika kuihabarisha jamii mambo mbalimbali yanayoendelea duniani.
“Si lazima Waandishi wote wa Habari waonekane kwenye Televisheni, kuna namna nyingi za kufanya kazi hii ikiwemo mitandao ya kijamii ambayo watumiaji wake wanaongezeka kwa kasi, kwa sasa dunia imehama kutoka mtaani kwenda mtandaoni.”  amefafanua Dkt. Abbasi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...