***********************************

Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Bw. Doto M. James na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah, Leo tar. 6 Aprili, 2021 wamewasili katika ofisi ndogo za Wizara Waterfront jijini Dar es salaam punde baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan katika hafla iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam.

Viongozi hawa wamepokelewa na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Prof, Kitila Mkumbo (Mb) ambapo wamepata nafasi ya kutambulishwa kwa Wakurugenzi na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara.

Katika Kikao hicho, Mhe. Prof. Kitila Mkumbo amewakaribisha katika Wizara ya Viwanda na Biashara huku akihaidi kufanya nao kazi kama timu moja katika kufikia malengo ya kuifanya nchi kuwa ya Viwanda ifikapo 2025.

Kwa upande wao Makatibu hao wamekubaliana kushirikiana na mawaziri ili kutimiza azma ya Mheshimiwa Rais ya Kukuza sekta ya Viwanda na Biashara nchini hasa katika kukuza pato la Taifa na Ajira kwa watanzania kwa kutunga sera na sheria ambazo ni rafiki kwa wawekezaji kuanzisha Viwanda vinavyochakata malighafi za ndani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...