Kiwanda kipya cha kutengeneza na kuunganisha Magari nchini Tanzania GF vehicles Assemblers (GFA) kilichopo Kibaha mkoani Pwani leo kimetimiza utengenezaji wa Gari ya miamoja (100)  kuanzia kipindi cha mwezi Januari hadi Aprili.

Akizungumza wakati wa sherehe za kuruhusu gari ya 100 kukanyaga aridhini baada ya kuunganishwa tayari kwa kutembea ,Meneja mkuu wa kiwanda hicho ,Ezra Mereng alisema ni kazi ngumu kukamilisha zoezi la uunganishaji na utengenezaji wa magari hayo kwa kuwa Tanzania sisi ndio Kiwanda cha kwanza kutengeneza (kuunganisha) magari .

Changamoto ni nyingi kutokana na kutokuwa na wataalamu wengi katika sekta hii ya Magari, lakini kwa kushirikiana na wataalamu wa nje tuliweza kuunganisha magari 10 ya awali na baadae wao wakaondoka na tukabaki na watanzani wenzetu ambao kwa uwezo wa Mungu leo tumefanikiwa kumaliza gari ya 100.

Pia alizitaka Tasisisi za serikali na kuagiza magari ambayo hayajaunganishwa na kazi ya kuunganisha ifanyike na viwanda vya ndani ili kukuza pato la taifa na kuongeza ajira kwa watanzania, pia kama nchi itajipatia fedha za kikgeni kwa kuuza nchi jirani Magari yanayotoka Tanzania.

Nae afisa masoko na manunuzai wa kampuni ya uuzaji wa magari ya FG Trucks & Equipments Ltd , Hamis Hasasn ambao ni moja ya wateja waliopeleka kazi ya kuunganishiwa Magari yao katika kiwanda hicho alisema,Mwanzo wateja walikuwa hawaamini kama magari hayo yatakuwa na ubora sawa lakini kwa kipindi hiki magari yapo mitaani na yanafanya vizuri,alisema Hamis na kuongeza kuwa kiwanda hicho kimeajiri Wafanyakazi 100  wenye ajira za kudumu, mikataba pamoja na za muda mfupi .

Meneja mkuu wa kiwanda cha kutengeneza Magari mapya cha Kwanza nchini Tanzania GF- Vehicle Assembly Ltd , Ezra Mareng akizungumza na wateja wa kiwanda hicho kilichopo Kibaha mkoani Pwan wakati wa sherehe ya kutimiza Magari 100 yaliotengenezwa na kiwanda hicho kwa kipindi Cha miezi Minne.




 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...