Mafunzo ya kudhbiti uadilifu kwa kamati za maadili kwa Tasisi za umma zilizopo jijini Arusha yameazinduliwa leo Makao makuu ya Tume ya Nguvu za Atomiki yaliyopo jijini Arusha. Ambapo washiriki wa mafunzo hayo wametakiwa kuhakikisha wanasimamia na kukuza maadili ya watumushi wa umma katika taasisi zao.

Wito huo umetolewa na Kaimu Mkurugenzi mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) Dk.Remigius Kawala wakati wa ufunguzi wa mafunzo  hayo ambapo amesema kuwa hatua ya kuwepo kwa kamati hizi za maadili katika taasisi za umma  ni lengo la serikali katika kujali na kusimamia maadili mema kwa wafanyakazi wake.

“Hizi kamati zinalengo la kusimamia madili mahala pa kazi na kuondoa ukosefu wa uadilifu kwa baadhi ya watumishi wa umma unaosababisha uwepo wa masuala mbali mbali yakiwemo vitendo vya rushwa, ulevi, uonevu, n.k. Hivyo naamini haya mtayajadili kwa kina katika kuleta ufumbuzi wake  huko kwenye kamati zenu” alisema Dk. Kawala.

Baadhi ya masuala yatakayojadiliwa kwenye mafunzo hayo ni pamoja na kanuni za maadili ya utumishi wa umma na namna ya kushughulikia malalamiko mbali mbali ya kimaadili,mkakati wa Taifa dhidi ya rushwa, dhana ya rushwa mahala pa kazi na dhana ya mgongano wa maslahi.

Taasisi zinazoshiriki mafunzo hayo ni pamoja na  CARMATEC, ATC, TEMDO na Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC).

Picha ya pamoja 
Baadhi ya Washiriki wa mafunzo hayo  wakifuatilia yaliyokuwa yakijadiliwa ukumbini humo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...