Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Damas D. Ndumbaro (Mb), amemsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Bi. Devotha Mdachi ili kupisha uchunguzi wa madai ya ubadhirifu wa fedha pamoja na masuala ya kiutawala yanayohusu Rasilimali Watu katika ofisi yake.
Kufuatia hatua hiyo Mhe. Waziri amemteua Betrita James Lyimo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi kutoka Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi hiyo hadi pale uchunguzi utakapokamilika.
Aidha, Dkt. Damas Ndumbaro ameielekeza Bodi ya Wakurugenzi ya TTB kuwasimamisha kazi watumishi wengine wanaohusika na tuhuma hizo kwa kuwa suala hilo lipo chini ya Mamlaka yao ili waweza kupisha uchunguzi dhidi ya madai yanayowakabili.
Hata hivyo, Waziri Dkt. Ndumbaro amesema maamuzi hayo hayahusiani na Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG). Uteuzi huo unaanza rasmi leo tarehe 10 Aprili, 2021.
Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Bi. Devotha Mdachi
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...