Na Chalila Kibuda, Michuzi Tv
WATANZANIA na wapenzi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wameendelea kumuenzi Hayati Dkt. John Magufuli na kusema kuwa hawatasahau mchango wake kwenye Nchi, huku wakimpongeza Rais Mama Samia Suluhu Hassan kwa kumudu vizuri nafasi hiyo na kuahidi kuendelea kusimamia miradi ya kimkakati.

Kauli hiyo ilitolewa Jijini Dar es Salaam jana na Kada wa CCM Charles Sabiniani wakati akitoa zawadi za kanga kwa vikundi mbalimbali vya Wanawake ikiwa ni jitihada za kumpongeza Rais Mama Samia Hassan Suluhu.
Sabiniani ambaye pia ni Mjasiliamali maalufu alisema kuwa anaguswa zaidi na uongozi wa mama na ndio maana ameamua kutoa zaidi hiyo.

Mmoja wa waliyepata Kanga hizo ni Anneth Kagenda, alisema kuwa anampongeza Rais Mama kwa kuongoza Nchi.

Alisema kuwa anamuombea kila la kheri kwa Mungu mama pamoja na Makamu wake Mhe. Mpango katika kuongoza Taifa.

Hata hivyo alitoa pongezi kwa Kada huyo kwa kumpatia zawadi ya kanga.


Kada za CCM Charles Sabinian pichani akiwa ametoa kanga kwa ajili ya kumpongeza Rais Mama Samia Hassan Suluhu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...