Nolasco Kilumile afisa kilimo wa halmashauri ya mji wa Njombe akifafanua na kutolea majibu baadhi ya changamoto za wakulima wa parachichi ikiwemo kuomba ushirikiano baina yao na serikali huku akisisitiza matumizi bora ya vipimo katika zao hilo ili kuepuka mkulima kuibiwa.
Mkurugenzi wa asasi inayohudumia wakulima wa Parachichi na kilimo hai mkoani humo NSHDA Ndugu Frenk Msigwa akifafanua namna asasi hiyo inavyoendelea kushirikiana na wakulia katika kutafuta masoko ya mazao yao ikiwemo kilimo cha parachichi.
Baadhi ya wakulima wa parachichi pamoja mazao mengine mkoani Njombe wakiwa katika mkutano wa wadau wa parachichi uliokutanisha wakulima wa zao hilo,makampuni na watalaamu wa serikali ulioandaliwa na asasi inayohudumia wakulima wa Parachichi na kilimo hai mkoani humo NSHDA na kumsikiliza afisa kilimo wa halmashauri ya mji wa Njombe mara baada ya kueleza changamoto zao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...