Na Amiri Kilagalila, Njombe
Halmashauri
ya Mji Njombe imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi milioni mia mbili
thelathini na tisa laki tisa na themanini elfu kwa vikundi 24, vikundi
08 vikiwa ni kwa vijana na vikundi 16 vya wanawake hii ikiwa ni
utekelezaji wa agizo la Serikali ambapo Halmashauri imeweza kutenga
asilimia kumi za mapato yake ya ndani kwa ajili ya zoezi hilo.
Akizungumza
wakati wa hafla ya makabidhiano ya hundi ya mfano Mwenyekiti wa
Halmashauri ya Mji Njombe Romanus Mayemba ameipongeza Halmashauri kwa
jinsi ambavyo imeweza kufanya usimamizi na kuhakikisha kwamba maagizo ya
Serikali ya utoaji mikopo bila riba yanatekelezwa katika kila robo na
kuwafikia walengwa kwa wakati.
“Niwapongeze
wale wote mliobahatika kupata mikopo.Fedha za mikopo zinazotolewa
zinajumuisha asilimia kumi ya mapato ya ndani pamoja na marejesho.
Unaporejesha mikopo unatoa fursa kwa vikundi vingine vyenye sifa kuweza
kukopa lakini pia unajijengea sifa ya kukopeshwa kwa mara nyingine.
Tuzingatie urejeshaji wa mikopo kwa wakati. Tunapokwenda kutumia mikopo
tuwe na uhakika wa kuirejesha na hii itatusaidia kusukuma maendeleo
kwenye Halmashauri yetu. Uaminifu ni jambo la msingi sana. Alisema
Mayemba
Kwa upande wake
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Bi. Illuminatha Mwenda amesema
kuwa Halmashauri imeweza kutoa mikopo mingi kutokana na ukusanyaji mzuri
wa mapato ya ndani jambo ambalo linapelekea ongezeko la utoaji mikopo
kila wakati na hivyo amewataka Wananchi kuhakikisha kuwa wanakuwa
wachangiaji wazuri wa mapato na kuwa wasimamizi kwa kuhakikisha kuwa
hakuna upotevu wa mapato kwani mafanikio hayo ni kutokana na makusanyo
ya mapato ya ndani kuwa mazuri.
Wakizungumza
kwa nyakati tofauti tofauti baadhi ya wawakilishi wa vikundi hivyo
wameipongeza Halmashauri kwa jitihada hizo na wameahidi kufanya kazi kwa
bidii ili kuweza kufanya marejesho na kupata fursa ya kuweza kukopeshwa
tena.
Kwa upande wake
Donas Innocent Kayombo mwakilishi kutoka kikundi cha Vijana Melinze
amesema kuwa changamoto kubwa wanayokabiliana nayo vijana kwenye
uundaji wa vikundi ni ukosefu wa shughuli ya pamoja jambo linalopelekea
vijana wengi kushindwa kujiunga kutokana na kuwa kila kijana anakuwa na
shughuli yake ya kujiongezea kipato na hivyo kuiomba Serikali kuweza
kuboresha miongozi hiyo ili kasi ya ukopaji kwa vijana iwe kubwa.
“Tulikuwa
tunasikia mitaani kuhusu mikopo. Tukaamua kuunda kikundi. Tuliomba
milioni kumi na tumepata kadri tulivyoomba na tunakwenda kuinuka
kiuchumi.”Alisema Kayombo
Naye
Rehema Nyezi mwakilishi kutoka kikundi cha wanawake amesema kuwa
wanaishukuru Halmashauri kwani wameweza kupatiwa mkopo kadri walivyoomba
na amesema kuwa lengo lao ni kwenda kuanzisha kilimo cha parachichi na
kuendeleza mradi wa ufugaji kuku na wameahidi kwenda kufanyia kazi fedha
hizo ili waweze kuzirejesha kwa wakati.
kwa
kipindi cha mwaka 2020/2021 Halmashauri imeweza kutoa mikopo yenye
thamani ya zaidi ya shilingi milioni mia tisa arobaini laki nane na
themanini kwa vikundi 96 ambapo 72 vya wanawake 22 vijana na 2
walemavu ikiwa ni mapato ya ndani ya Halmashauri na fedha za marejesho.
Rai imeendelea kutolewa kwa watu wenye ulemavu kuchangamkia fursa ya
ambapo kwa sasa kumekuwa na mabadiliko ya idadi ya wanaojiunga ambapo
hata mlemavu mmoja anaweza kuomba na kupatiwa mkopo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...