Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkta.Damas Ndumbaro ( katikati) akiwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Mary Masanja wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt.Allan Kijazi mara baada ya kutembelea Shamba la kutunzia  Wanyamapori yatima na  waliojeruhiwa la Makoa lililopo wilayani Hai mkoani Kilimanjaro ambapo  Wizara imetoa siku saba kwa Uongozi wa mkoa kurekebisha kasoro za mikataba ya shamba hilo walioingia na Mwekezaji
Mwanzilishi wa Shamba la kutunzia Wanyamapori Yatima na waliojeruhiwa la Makoa,  Elizabeth Stigmaller akitoa maelezo kwa Viongozi wakuu wa  Wizara ya Maliasili na Utalii wakiwa na Mwenyeji wao Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Anna Mghwira walipotembelea leo  shamba hilo na kujionea wanyamapori mbalimbali wanaolelewa  ndani ya shamba hilo mkoani hapo
Mhudumu wa shamba la kutunzia Wanyamapori Yatima na waliojeruhiwa la Makoa, Jeremia Nyalale akiwamwagia maji  tembo  ili kupoza kiwango cha joto katika miili yao.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkta.Damas Ndumbaro ( katikati) akiwa na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Anna Mghwira  pamoja na Mbunge wa Hai, Saashisha Mafuwe ( watatu kushoto)  wakimsikiliza Katibu Tawala wa wilaya ya Hai, Upendo Wella kabla ya kuanza kutembelea Shamba la kutunzia  Wanyamapori yatima na  waliojeruhiwa la Makoa lililopo wilayani Hai mkoani Kilimanjaro ambapo  Wizara imetoa siku saba kwa Uongozi wa mkoa kurekebisha kasoro za mikataba ya shamba hilo walioingia na Mwekezaji. Mbele ni  Mwanzilishi wa Shamba la kutunzia Wanyamapori Yatima na waliojeruhiwa la Makoa,  Elizabeth Stigmaller
Mwanzilishi wa Shamba la kutunzia Wanyamapori Yatima na waliojeruhiwa la Makoa,  Elizabeth Stigmaller (wa kwanza kulia) akitoa maelezo kwa Viongozi wakuu wa  Wizara ya Maliasili na Utalii akiwemo Waziri wa Wizara hiyo,Dkt,Damas Ndumbaro pamoja na Naibu Waziri wa wizara hiyo,Mhe, Mary Masanja ( wa kwanza kulia)  wakiwa na Mwenyeji wao Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Anna Mghwira (mbele) walipotembelea leo  shamba hilo na kujionea wanyamapori mbalimbali wanaolelewa  ndani ya shamba hilo mkoani hapo
Mhudumu wa shamba la kutunzia Wanyamapori Yatima na waliojeruhiwa la Makoa, Jeremia Nyalale akiwa naye  mtoto yatima tembo akimfuata wakati  Viongozi wakuu wa  Wizara ya Maliasili na Utalii akiwemo Waziri wa Wizara hiyo,Dkt,Damas Ndumbaro pamoja na Naibu Waziri wa wizara hiyo,Mhe, Mary Masanja  wakiwa na Mwenyeji wao Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Anna Mghwira walipotembelea leo  shamba hilo na kujionea wanyamapori mbalimbali wanaolelewa  ndani ya shamba hilo lililopo wilayani Hai mkoani Kilimanjaro
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkta.Damas Ndumbaro ( wa pili kushoto) akiwa na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Anna Mghwira 9 watatu kushoto)  wakiwa na viongozi mbalimbali wakiangalia    Wanyamapori yatima na  waliojeruhiwa katika shamba la Makoa  lililopo wilayani Hai mkoani Kilimanjaro . Wa kwanza kushoto  Mwanzilishi wa Shamba la kutunzia Wanyamapori Yatima na waliojeruhiwa la Makoa,  Elizabeth Stigmaller 
(PICHA ZOTE NA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
**************************************
WIZARA ya Maliasili na Utalii imetoa muda wa siku saba kwa uongozi wa mkoa  wa Killimanjaro  kuhakikisha unarekebisha kasoro zilizo kwenye mikataba ya shamba la kutunzia wanyamapori  yatima la Makoa kabla ya kupewa kibali cha kuleta Simba kutoka nje ya nchi kwa ajili ya matunzo. 
Akizungunza mara baada ya kutembelea shamba  la  Wanyamapori la Makoa , Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Damas Ndumbaro amesema kuwa  shamba hilo linapokea wanyamapori  yatima na majeruhi kutoka kwenye hifadhi zote hapa  nchini. 
Amesema kutokana na umuhimu wa shamba hilo, ipo haja  ya Serikali ya Mkoa kusaidia  Chama cha Ushirika cha  Urudu Makoa ili kiweze kufahamu  namna sahihi ya kuingia mikataba yenye tija  kwa Taifa. 
“Nimetoa siku saba kwa viongozi wa Mkoa kuhakikisha  wanakisaidia Chama  cha Ushirika cha Uduru Makoa  ili waweze kurekebisha kasoro zilizojitokeza kwenye mikataba ya uwekezaji pia wafahamu, ukomo wa mikataba na nani wanaingia nae mikataba hiyo na manufaa yake kwa vyama vya ushirika na Taifa kwa ujumla,” Amesisitiza Dkt. Ndumbaro.
Aidha, amesema  ziara  yake  imelenga kutazama bustani hiyo inayotunza wanyamapori waliojeruhiwa au yatima ambao hutunzwa hadi na baadaye  kurudishwa kwenye hifadhi pindi wanapokuwa au kurejea katika hali zao za kawaida. 
Dkt. Ndumbaro amesema kuwa Wizara imejiridhisha  pasipo shaka malezi na mazingira ya  utunzaji  wa wanyamapori  hao  yanaridhisha licha yakuwa bado kuna ukakasi katika mikataba waliyoingia. 
” Mkataba walioingia kati  ya Makoa na Mwekezaji huyo  haijafuata misingi ya kisheria na leseni iliyotolewa imetolewa kwa mtu binafsi ambaye si muhusika  wa shamba hilo, hivyo tumewaagiza Mkoa  kukamilisha kasoro hizo mara moja,  wakikamilisha  taratibu zote walete maombi yao yakuleta wanyamapori kutoka  nje ya nchi  tutayashughulikia, “amesema Dkt. Ndumbaro.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Anna Mghwira  amesema kumekuwa na ukakasi wa kufahamu Mwekezaji halisi ni nani ili kuingia mkataba jambo ambalo baada ya Waziri kufika  kila kitu kimekuwa wazi. 
” Muda wa siku saba tuliopewa unajitosheleza  maana kila kitu kipo ni kiasi cha kujipanga kulingana na Sheria na taratibu kwa mwongozo wa wataalamu wetu,” amesema 
Naye mbunge wa jimbo hilo Mhe. Saashisha Mafuwe amesema ujio wa Waziri Ndumbaro umesaidia kufungua  ukurasa mpya  wa utendaji wa vyama vya  ushirika vianze kuingia mikataba itakayoleta mabadiliko na faida kwa Taifa. 
“Ombi langu kwa Mawaziri wengine kufika jimboni hapa kwani upo umuhimu mkubwa wa Serikali kutupia jicho la pekee  hasa katika  mikataba ya vyama vya ushirika,” amesema Mhe. Saashisha
Kwa upande wake,  Mwenyekiti wa Chama cha Ushirika Uduru Makoa,Saeli Mafuwe amesema wamepokea maelekezo na maagizo ya wizara husika na watayafanyia kazi kwa mujibu wa taratibu, kanuni na sheria. 
” Mkataba wetu unakataza Mwekezaji kumpangisha Mwekezaji mwingine, na hapa ndicho kilichotokea, tutakaa na timu ya wataalamu kutoka wilayani na mkoani, ili kuona namna ya kutatua matatizo haya,” 
Katika ziara hiyo  walikuwepo Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja, Katibu Mkuu, Dkt. Allan Kijazi na Wataalamu mbali mbali kutoka Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii ambazo ni TAWIRI, TAWA na TANAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...