Waziri wa Maliasili na Utalii,
Dkta.Damas Ndumbaro ( katikati) akiwa na Naibu Waziri wa Maliasili na
Utalii, Mhe.Mary Masanja wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,
Dkt.Allan Kijazi mara baada ya kutembelea Shamba la kutunzia
Wanyamapori yatima na waliojeruhiwa la Makoa lililopo wilayani Hai
mkoani Kilimanjaro ambapo Wizara imetoa siku saba kwa Uongozi wa mkoa
kurekebisha kasoro za mikataba ya shamba hilo walioingia na Mwekezaji
Mwanzilishi wa Shamba la
kutunzia Wanyamapori Yatima na waliojeruhiwa la Makoa, Elizabeth
Stigmaller akitoa maelezo kwa Viongozi wakuu wa Wizara ya Maliasili na
Utalii wakiwa na Mwenyeji wao Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Anna
Mghwira walipotembelea leo shamba hilo na kujionea wanyamapori
mbalimbali wanaolelewa ndani ya shamba hilo mkoani hapo
Mhudumu wa shamba la kutunzia
Wanyamapori Yatima na waliojeruhiwa la Makoa, Jeremia Nyalale
akiwamwagia maji tembo ili kupoza kiwango cha joto katika miili yao.
Waziri wa Maliasili na Utalii,
Dkta.Damas Ndumbaro ( katikati) akiwa na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,
Mhe. Anna Mghwira pamoja na Mbunge wa Hai, Saashisha Mafuwe ( watatu
kushoto) wakimsikiliza Katibu Tawala wa wilaya ya Hai, Upendo Wella
kabla ya kuanza kutembelea Shamba la kutunzia Wanyamapori yatima na
waliojeruhiwa la Makoa lililopo wilayani Hai mkoani Kilimanjaro ambapo
Wizara imetoa siku saba kwa Uongozi wa mkoa kurekebisha kasoro za
mikataba ya shamba hilo walioingia na Mwekezaji. Mbele ni Mwanzilishi
wa Shamba la kutunzia Wanyamapori Yatima na waliojeruhiwa la Makoa,
Elizabeth Stigmaller
Mwanzilishi wa Shamba la
kutunzia Wanyamapori Yatima na waliojeruhiwa la Makoa, Elizabeth
Stigmaller (wa kwanza kulia) akitoa maelezo kwa Viongozi wakuu wa
Wizara ya Maliasili na Utalii akiwemo Waziri wa Wizara hiyo,Dkt,Damas
Ndumbaro pamoja na Naibu Waziri wa wizara hiyo,Mhe, Mary Masanja ( wa
kwanza kulia) wakiwa na Mwenyeji wao Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe.
Anna Mghwira (mbele) walipotembelea leo shamba hilo na kujionea
wanyamapori mbalimbali wanaolelewa ndani ya shamba hilo mkoani hapo
Mhudumu wa shamba la kutunzia Wanyamapori Yatima na
waliojeruhiwa la Makoa, Jeremia Nyalale akiwa naye mtoto yatima tembo
akimfuata wakati Viongozi wakuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii
akiwemo Waziri wa Wizara hiyo,Dkt,Damas Ndumbaro pamoja na Naibu Waziri
wa wizara hiyo,Mhe, Mary Masanja wakiwa na Mwenyeji wao Mkuu wa Mkoa wa
Kilimanjaro, Mhe. Anna Mghwira walipotembelea leo shamba hilo na
kujionea wanyamapori mbalimbali wanaolelewa ndani ya shamba hilo
lililopo wilayani Hai mkoani Kilimanjaro
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkta.Damas Ndumbaro ( wa
pili kushoto) akiwa na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Anna Mghwira 9
watatu kushoto) wakiwa na viongozi mbalimbali wakiangalia
Wanyamapori yatima na waliojeruhiwa katika shamba la Makoa lililopo
wilayani Hai mkoani Kilimanjaro . Wa kwanza kushoto Mwanzilishi wa
Shamba la kutunzia Wanyamapori Yatima na waliojeruhiwa la Makoa,
Elizabeth Stigmaller
(PICHA ZOTE NA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
**************************************
WIZARA ya Maliasili na Utalii
imetoa muda wa siku saba kwa uongozi wa mkoa wa Killimanjaro
kuhakikisha unarekebisha kasoro zilizo kwenye mikataba ya shamba la
kutunzia wanyamapori yatima la Makoa kabla ya kupewa kibali cha kuleta
Simba kutoka nje ya nchi kwa ajili ya matunzo.
Akizungunza mara baada ya
kutembelea shamba la Wanyamapori la Makoa , Waziri wa Maliasili na
Utalii, Dkt. Damas Ndumbaro amesema kuwa shamba hilo linapokea
wanyamapori yatima na majeruhi kutoka kwenye hifadhi zote hapa
nchini.
Amesema kutokana na umuhimu wa
shamba hilo, ipo haja ya Serikali ya Mkoa kusaidia Chama cha Ushirika
cha Urudu Makoa ili kiweze kufahamu namna sahihi ya kuingia mikataba
yenye tija kwa Taifa.
“Nimetoa siku saba kwa viongozi
wa Mkoa kuhakikisha wanakisaidia Chama cha Ushirika cha Uduru Makoa
ili waweze kurekebisha kasoro zilizojitokeza kwenye mikataba ya
uwekezaji pia wafahamu, ukomo wa mikataba na nani wanaingia nae mikataba
hiyo na manufaa yake kwa vyama vya ushirika na Taifa kwa ujumla,”
Amesisitiza Dkt. Ndumbaro.
Aidha, amesema ziara yake
imelenga kutazama bustani hiyo inayotunza wanyamapori waliojeruhiwa au
yatima ambao hutunzwa hadi na baadaye kurudishwa kwenye hifadhi pindi
wanapokuwa au kurejea katika hali zao za kawaida.
Dkt. Ndumbaro amesema kuwa
Wizara imejiridhisha pasipo shaka malezi na mazingira ya utunzaji wa
wanyamapori hao yanaridhisha licha yakuwa bado kuna ukakasi katika
mikataba waliyoingia.
” Mkataba walioingia kati ya
Makoa na Mwekezaji huyo haijafuata misingi ya kisheria na leseni
iliyotolewa imetolewa kwa mtu binafsi ambaye si muhusika wa shamba
hilo, hivyo tumewaagiza Mkoa kukamilisha kasoro hizo mara moja,
wakikamilisha taratibu zote walete maombi yao yakuleta wanyamapori
kutoka nje ya nchi tutayashughulikia, “amesema Dkt. Ndumbaro.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa
Kilimanjaro Mhe. Anna Mghwira amesema kumekuwa na ukakasi wa kufahamu
Mwekezaji halisi ni nani ili kuingia mkataba jambo ambalo baada ya
Waziri kufika kila kitu kimekuwa wazi.
” Muda wa siku saba tuliopewa
unajitosheleza maana kila kitu kipo ni kiasi cha kujipanga kulingana na
Sheria na taratibu kwa mwongozo wa wataalamu wetu,” amesema
Naye mbunge wa jimbo hilo Mhe.
Saashisha Mafuwe amesema ujio wa Waziri Ndumbaro umesaidia kufungua
ukurasa mpya wa utendaji wa vyama vya ushirika vianze kuingia mikataba
itakayoleta mabadiliko na faida kwa Taifa.
“Ombi langu kwa Mawaziri wengine
kufika jimboni hapa kwani upo umuhimu mkubwa wa Serikali kutupia jicho
la pekee hasa katika mikataba ya vyama vya ushirika,” amesema Mhe.
Saashisha
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa
Chama cha Ushirika Uduru Makoa,Saeli Mafuwe amesema wamepokea maelekezo
na maagizo ya wizara husika na watayafanyia kazi kwa mujibu wa taratibu,
kanuni na sheria.
” Mkataba wetu unakataza
Mwekezaji kumpangisha Mwekezaji mwingine, na hapa ndicho kilichotokea,
tutakaa na timu ya wataalamu kutoka wilayani na mkoani, ili kuona namna
ya kutatua matatizo haya,”
Katika ziara hiyo walikuwepo
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja, Katibu Mkuu,
Dkt. Allan Kijazi na Wataalamu mbali mbali kutoka Taasisi zilizo chini
ya Wizara ya Maliasili na Utalii ambazo ni TAWIRI, TAWA na TANAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...