Na Mwandishi wetu, Simanjiro

DIWANI mstaafu wa Kata ya Naisinyai Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, Clempu Ole Kinoka ameshinda kesi na kurudishiwa shamba lake la zaidi ya ekari 1,000 lililopo mpakani mwa Kijiji cha Langai na Naberera.

Clempu ameshinda kesi hiyo iliyokuwa kwenye mahakama Kuu ya Mkoa wa Arusha, dhidi ya mfugaji Lenginyu Yamat.Hata hivyo, Mahakama hiyo imeagiza Lenginyu aachalie shamba hilo mara moja na kulipa faini ya shilingi milioni 120.

Klempu ameishukuru Mahakama hiyo kwa kutoa haki yake kwani shamba hilo alipata kihalali kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu.Amesema mgogoro kwenye shamba hilo ulianza tangu mwaka 2019 na baadhi ya wanasiasa walichochea ili waichukue ardhi hiyo.

"Namshukuru Mungu nimefanikiwa kupata tena shamba langu ambalo nilinunua kwa njia ya halali kwa kufuata sheria tangu awali," amesema Clempu.Mfanyabiashara wa Naisinyai, Siria Ngodedia amesema anamshukuru Mungu kwani Mahakama imetenda haki na kurejesha ardhi hiyo kwa Diwani huyo mstaafu.

"Haki ya mtu haiwezi kwenda bure, Mahakama imeona mahali haki inapaswa kuwepo, tunamshukuru Mungu kwa hilo kwani mzee amerudishiwa eneo lake na kazi iendelee," amesema Siria.Mkazi wa kijiji cha Langai, Ernest Martini amesema siasa chafu ilitaka kutumika ili kumdhulumu Clempu eneo lake kwani alinunua kihalali shamba hilo.

"Baadhi ya viongozi walitumika vibaya na kutaka kudhulumu mali ya Diwani huyo mstaafu wa kata ya Naisinyai ila Mahakama imetenda haki," amesema.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...