Na Mwandishi wetu, Michuzi TV

KATIBU  wa Itikadi na Uenezi, wa Chama cha Mapinduzi CCM , Shaka Hamdu Shaka, amesema kupitia agizo la Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo la kumtaka atoe namba ya simu yake kwa wananchi kwa ajili ya kupokea kero na changamoto mbalimbali za wananchi tayari amepokea kero  hizo za wananchi kwa njia mbalimbali za mtandao.

Amesema kwa takribani muda wa siku moja na masaa kadhaa amepokea ujumbe mfupi kwa njia ya kawaida jumbe 2974 za kero  na changamoto  na ujumbe wa njia ya WhatsApp amepokea  jumbe 2664.

Akizungumza  mkoani Dar es Salaam wakati wa mapokezi ya kumpokea Katibu Mkuu wa Chama hicho Taifa, Daniel Chongolo na Sekretarieti yake ya Halmashauri kuu, amesema  jumbe hizo alizopokea  zilizokuwa na  viambatanisho na vielelezo vya kero mbalimbali za wananchi. 

Shaka  amesema hiyo inaashiria kwamba  Sekretarieti  hiyo na Chama chao wanayokazi yakufanya hivyo amehaidi kuanza kuzishughulikia huku akiwataka watendaji wa chama na serikali kuzifanyia kazi changamoto hizo, kila mmoja kwa nafasi yake  atimize wajibu wake kwa nafasi yake.

"Nataka niwahakikishie watanzania kuwa Sekretarieti hii imebeb maono na imebeba mtazamo ipo tayari kutekeleza kwa vitendo adhima  na nia ya Rais Samia Suluhu Hassan,"amesema na kuongeza,

"Tunakwenda kusimamia kero,changamoto, haki na dhuruma kuwahakilishia watanzania wanafikia mwisho wake kwani Rais Samia Suluhu Hassan aliwahi kusema Uongozi ni kuonyesha nia na sio kufunga njia,"amesema.

Amewataka viongozi wa Serikali walioteuliwa kufanya kazi kwa bidii kwani, wakati huu wanapaswa kujituma kuhakikisha kazi inaendelea.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...