Ushauri huo umetolewa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. Lughano
J.M. Kusiluka, kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu
Mzumbe na Sokoine wakati akifungua Kongamano
la Career Fair 2021, lililodhaminiwa na Benki ya NMB kwa ushirikiano na Shirika
la AIESEC Tanzania.
Prof. Kusiluka amesema kongamano la “Career Fair” kwa mwaka
2021 limekuja wakati muafaka, kutokana na changamoto mbalimbali zinazowakabili
vijana, hususani suala la ukosefu wa
ajira pindi wanapohitimu masomo yao.
Amesema “Kasi ya mabadiliko ya teknolojia duniani na ukosefu
wa ajira kwa vijana ni changamoto kubwa ambayo imeendelea kutuumiza vichwa katika
kupambanua nini hatma ya wahitimu wetu, na
kwamba hatuna budi kubadilisha mfumo wa ufundishaji ili uendane na mahitaji
halisi ya soko, ya kuzalisha
wataalamu wabobevu na wabunifu, ambao wataweza kujiajiri wenyewe mara wanapohitimu,
badala ya kusubiri kuajiriwa”. alisisitiza
Ameipongeza Benki
ya NMB na Shirika la AIESEC, kwa uwekezaji mkubwa walioufanya kwa vijana
kupitia programu ya “Career Fair” ambayo imelenga kumjenga na kumkomboa kijana kifikra.
Ameahidi Chuo Kikuu Mzumbe kuendelea kubuni mikusanyiko ya aina hiyo yenye
kulenga kuwajengea uwezo vijana na fursa zilizopo; pamoja na kuendeleza mpango
wake wa kuimarisha kituo cha kuatamia bunifu za wanafunzi chini ya Skuli ya
Biashara, kwa lengo la kuwaanda vijana
kujiajiri.
Akizungumza wakati
wa Kongamano hilo, Mkuu wa Kanda ya Mashariki NMB, Ndugu. Dismas Prosper, amesema Benki ya NMB imedhamini
Kongamano hilo ili kutoa mafunzo ya kuwajengea uwezo vijana, kuibua vipaji na kufungua
fursa za mafunzo ya kazi kupitia programu yake ya ” Career development” ambayo
inatoa fursa kwa vijana waliohitimu vizuri mafunzo yao kupata uzoefu wa
kazi na hata kuajiriwa katika benki hiyo
kulingana na fursa zilizopo.
Amesema hadi sasa chini ya mpango huo Benki ya NMB imewawezesha zaidi ya vijana
50 kujengewa uwezo, kupata ujuzi na kujifunza kazi kwa vitendo, huku baadhi yao
wakiwa wameajiriwa na Benki hiyo kwa nafasi mbalimbali.
“ Programu hii tutaiendeleza kwa vyuo vikuu vyote nchini kwa lengo la
kuibua vipaji na ubunifu ili tutimize azma yetu ya kuendelea kuwa Benki Bora ya
vijana” alisisitiza.
Naye Mkurugenzi wa Shirika la AIESEC Tawi la Tanzania, Bw. Michael Chacha, amesema Shirika lake litaendelea kuwajengea uwezo vijana wahitimu wa Elimu ya Juu ili kusaidia kupunguza changamoto za ajira pamoja na kuendelea kutoa mafunzo ya namna mbalimbali kwa vijana kupia washirika wake wa ndani na nje, ili kuandaa viongozi wenye uwezo kusaidia maendeleo ya Taifa.
Kongamano la “ Career Fair” limefanyika Chuo Kikuu Mzumbe -Morogoro,
na kuwashirikisha vijana zaidi 1000, ambao walipata fursa ya kujifunza mambo mbalimbali
kuhusu ujasiriamali, uongozi, biashara ajira, ubunifu na Teknolojia. Mafunzo
hayo yalitolewa na wataalamu mbalimbali wakiwemo wa Benki ya NMB na AIESEC Tanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...