Benki ya CRDB na Mfuko wa Bima ya Taifa NHIF imeendelea na utekelezaji
wa tumeanza utekelezaji wa mpango wa “Ushirika Afya” kwa kuingia
makubaliano na Chama Kikuu cha Ushirika cha maziwa mkoani Tanga kwa
ajili ya kuwapatia bima ya afya wanachama wake mkoani humo ambao ni
wazalishaji wa maziwa kama sehemu ya mpango wa Ushirika Afya.
Mgeni Rasmi wakati wa Kuingia Makubaliano hayo Mkuu wa Wilaya ya Tanga
Mh. Thobias Mwilapwa amewapongeza benki ya CRDB na Mfuko wa Bima ya afya
ya Taifa kwa Ubunifu wa mpango huo ambao utawafaidisha wakulima wengi
nchini “ Nasihi wanaushirika katika mkoa wa Tanga Kutumia Fursa hii
tujiunge kwa wingi kwenye vyama vya ushirika ili kutumia fursa hii
kuboresha maisha ya familia zetu” Mh. Mwilapwa
Kwa niaba ya Benki ya CRDB Afisa Biashara Mkuu Dkt. Joseph Witts
alisema Katika Makubaliano hayo Benki ya CRDB itawawezesha wanachama wa
chama kikuu kulipia bima ya Afya bila riba yoyote na hivyo kuboresha
uzalishaji wa maziwa katika mkoa wa Tanga.” Huu ni mpango maalumu wa
Benki yetu unaolenga kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya katika
maisha ya wateja wetu walioko kwenye sekta ya Kilimo nchini kote”
alieleza Dkt. Witts.
Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa NHIF Bw. Christopher Mapunda alisema
kuwa mfuko wa Bima ya taifa katika mkakati huu unalenga kuboresha
upatikanaji wa huduma za Afya kwa wakulima na wafugaji nchini. “Mpango
utawawezesha wazalishaji wa maziwa kupata huduma za afya katika vituo
zaidi ya Elfu nane katika nchi nzima” alieleza Bw. Mapunda
Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika wa maziwa mkoani Tanga Nd. Shamte
Said amewashukuru Benki ya CRDB na NHIF kwa kuja na mpango huo “
Nawapongeza kwa kuwakumbuka wazalishaji wa maziwa nawahidi tutatumia
fursa hii kujihakikishia upatikanaji wa matibabu” Ndg. Shamte
Hafla ya utiaji sahihi wa makubaliano hayo ulihudhuriwa na Mrajisi
Msaidizi wa vyama vya Ushirika Mkoa wa Tanga, Maafisa wa Mfuko wa Bima
ya Taifa, Maafisa wa Benki ya CRDB na Wajumbe Wa Bodi ya Chama Kikuu cha
Ushirika wa Maziwa Tanga.
Utekelezaji wa mpango wa Ushirika Afya ulianza mapema wiki iliyopita
ambapo Benki ya CRDB na NHIF waliingia mkataba wa makubaliano na na
vyama vya ushirika vya CHUTCU kilichopo wilaya ya Chunya, vyama vya MCU
na MWAMARU vilivyopo wilaya ya Rungwe, Mbeya.
Katika mpango huu Benki ya CRDB inasidia kurahisisha upatikanaji wa bima
za afya kwa wakulima waliopo katika vyama vya ushirika (AMCOS) kupitia
huduma ya mkopo wa gharama za bima iliyopewa jina "Ushirika Afya Premium
Loan." Huduma hiyo inatolewa bila makato wala riba. Mkulima anaruhusiwa
kukata bima yake, pamoja na wategemezi wake ikiwamo mke/ mume na
watoto.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...