Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi  Evarist Ndikilo wa kati kati aliyenyoosha mikono akizungumza na baadhi ya  wawakilishi (Delegation) kutoka Chemba ya Wafanyabiashara wa Kichina Tanzania (Chinese Business Chamber in Tanzania) kwa ajili ya kujadili mambo mbali mbali ikiwemo kupanga mikakati ya ujenzi wa viwanda katika Mkoa huo.
Baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Pwani wakiwa katika kikao hicho cha pamoja na Wawakilishi (Delegation) kutoka Chemba ya Wafanyabiashara wa Kichina Tanzania (Chinese Business Chamber in Tanzania) ambao walifika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya kupata ardhi kwa ajili ya ujenzi uwekezaji wa viwanda.


Na Victor Masangu, PWANI

SERIKALI ya Mkoa wa Pwani katika kuhakikisha inatekeleza kwa vitendo  azma ya kuwa na uchumi wa viwanda na kuwapa fursa wawekezaji  wa ndani na nje ya nchi imekutana na baadhi Wawakilishi (Delegation) kutoka Chemba ya Wafanyabiashara wa Kichina Tanzania (Chinese Business Chamber in Tanzania) kwa lengo la kujadili na kupanga mikakati ya kupata ardhi kwa ajili ya ujenzi wa viwanda.

Katika kikao hicho ambacho kiliongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani na kuhudhuliwa na baadhi ya viongozi mbali mbali wa Mkoa lengo ikiwa ni kufanya mazungumzo na wawakilishi hao kwa ambayo yataweza kuleta mabadiliko chanya  ya kimaendeleo kupitia sekta ya uwekezaji wa viwanda mbali mbali ambavyo vikikamilika vitaweza kuwa mkombozi mkubwa kwa wananchi katika  kutoa fursa za ajira na kukuza uchumi.

 Akizungumza katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo alibainisha kwamba lengo kubwa la ujio wa wawakilishi hao ni kuweza  kutafuta eneo la ardhi kwa ajili ya Ujenzi wa Viwanda ikiwa ni kutekeleza maombi waliyowasilisha kwa Mhe Rais walipokutana na kufanya mazungumzo Aprili, 21 mwaka  2021.

“Tumepokea ugeni huu  na katika mazungumzo yao ujumbe huo umekuja kwa lengo kutafuta Ardhi kwa ajili ya Ujenzi wa Viwanda ikiwa ni kutekeleza maombi waliyowasilisha kwa Mhe Rais walipokutana na kufanya mazungumzo hivi karibuni kwa hiyo sisi kama Mkoa wa Pwani suala hili tutalifanyia kazi ili kuwapatia ardhi ya kujenga viwanda,”alisema Ndikilo.

Aidha katika hatua nyingine  Ndikilo  amewatoa hofu kwa kuwahakikishia wawakilishi hao wa wafanyabiashara kuwa Mkoa  bado una maeneo ambayo tayari yametengwa  maalumu kwa ajili ya Ujenzi wa Viwanda hivyo watahakikisha wanawapa ushirikiano wa kutosha katika kila hatu ili waweze kutimiza malengo waliyojiwekea.


Pia Ndikilo  amependekeza  kwa Wawekezaji hao kuwekeza  kwenye eneo la Kwala ambalo Jumla ya Hekta 500 wanazohitaji zitapatikana, na kuwaeleza kuwa  eneo la Kwala linafaa kwa Uwekezaji huo wa ujenzi wa Viwanda (Industrial Park).

Katika hatua nyingine alifafanua kuwa katika eneo la Kwala kwa sasa lina Miundombinu mbinu yote Muhimu ikiwemo, Maji ya uhakika, Barabara, Umeme wa uhakika ukaribu na Bandari kavu, ukaribu wa Reli ya Mwendokasi, na ukaribu na Jiji la Dar es salaam.

Wawekezaji hao wakiongozwa na Bw. Janson Huang  wameeleza kuwa wanategemea kujenga na kuanzisha viwanda  zaidi ya 200 vya kuzalisha bidhaa mbali ikiwemo madawa, Kuunganishia pikiki, Viyoyozi, simu za mikononi  hivyo hitaji lao la kwanza ni Ardhi ila waendelee na michakato mingine ya Uwekezaji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...