Na.Ashura Mohamed-Arusha

Serikali  Mkoani  Arusha imesema kuwa itaendelea kusaidia sekta binafsi ili ziendelee kufanya vizuri kwa kuwa zimekuwa zikiisaudia Serikali kutoa ajira.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kiwanja kipya Cha burudani  maarufu kama Tanzanite Lounge kilichopo eneo la fire daraja mbili Mkoani Arusha,Msaidizi wa mkuu wa wilaya ya Arusha Mjini Enock Philip Mkumbwa ambaye alimwakilisha Mkuu  wa wilaya ya Arusha mjini  Kenani Kihongosi,alisema kuwa Serikali itaendelea kutoa ushirikiano wa kutosha na kuwawezesha wafanyabiashara na wawekezaji katika sekta hiyo binafsi kufanya shughuli zao katika mazingira wezeshi na rafiki.

"Hawa ni watu mihimu mno kwa kukuza Uchumi wa wilaya yetu na  mkoa wetu na tunapaswa kuwapa ushirikiano kwa kuhakikisha kuwa Usalama unakuwepo na mazingira ya kufanya biashara yanakuwa wezeshi kwa kuwa wanatusaidia sana,kutoa ajira na wanalipa Kodi"alisema Bw.Enock

Alisema serikali wilayani hapo itaendelea kufanya kazi kwa ukaribu na kuhakikisha changamoto ndogo ndogo ambazo zinawakwamisha wafanyabiashara zinakwisha kabisa,kwa Kasi ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Raisi Mh.Samia Suluhu Hassan.

"Niwatake tu Wamiliki wa Tanzanite Lounge muhakikishe kuwa mnatoa huduma bora na za viwango kwa kuwa mpo katika ushindani ili basi kesho na keshokutwa tusikie  kuwa mnawekeza katika eneo jingine kwa manufaa ya wananchi wetu na Taifa kwa ujumla"Alisisitiza bw.Mkumbwa.

Aidha aliwataka Wakazi wa wilaya ya Arusha na mkoa kwa ujumla, kuhakikisha kuwa wanatembelea eneo hilo kwaajili ya kupata burudani mbalimbali,Vyakula vya Asili ili kutoa mchango kwa mwekezaji huyo.

Nae Mkurugenzi wa Tanzanite Lounge bw.Mark Matolo alisema kuwa wamewekeza katika sekta hiyo ya burudani kwa kuwa jiji la Arusha ni moja ya majiji yenye sifa zake ikiwa ni pamoja na utalii,hivyo kuwataka Wakazi wa Jiji la Arusha na viunga vyake kuhakikisha wanafika katika eneo hilo kupata ladha tofauti tofauti.

Bw.Mark alisema kuwa wamejipanga katika kuhakikisha kuwa wanaendelea kutoa mchango wao katika sekta hiyo ya burudani kwa kuhakikisha kuwa wanatoa huduma bora zaidi zenye viwango na kila mtu atakayefika eneo hilo kuendelea kutamani kufika katika eneo hilo.

"Tumejipanga vyema na tumeangalia soko linahitaji nini haswa kwa mkoa wetu wa Arusha,kuna vyakula vya asili,kuna vitu vya kuchoma choma Kama kuku na Nyama ya ng'ombe ,mbuzi na burudani hapa patakuwa ndio nyumbani."Alisema Mark

Niwasisitize tu Wakazi wa mkoa wa Arusha na wageni ambao huwa wanatembelea mkoa wetu kuhakikisha kuwa wanafika eneo hili kupata huduma zetu,na tumejipanga vyema kuliko ambavyo wanadhani.

Muonekano wa ndani wa club ya Tanzanite Lounge
Msanii wa kizazi kipya Joh Makini mwamba wa kaskazini ambaye nae alihudhuria tukio Hilo la uzinduzi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...